Na Mwandishi wetu-Mahakama ya Tanzania
Msajili
Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma amewahimiza watumishi wa
Mahakama kuzingatia maadili na kuenzi utamaduni wa Mahakama, ikiwemo kuvaa mavazi
(dress code) yanayokubalika na yaliyoelekezwa na nyaraka mbalimbali za utumishi
wa umma.
Mhe.
Chuma alitoa agizo hilo jana tarehe 27 Oktoba, 2022 wakati wa ziara yake ya
kikazi katika Kituo cha Mahakama ya Mwanzo Manundu iliyopo Wilaya ya Korogwe mkoani
Tanga.
"Watumishi
wa Mahakama wanapaswa kuvaa mavazi ambayo yanazingatia utamaduni wa Mahakama na
mwongozo wa mavazi kwa watumishi wa umma, wanapokuwa kazini wakitekeleza
majukumu yao ya utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi,"alisisitiza.
Mhe.
Chuma alisema kuwa watumishi wa Mahakama wanatakiwa kuwa kioo katika jamii
katika mambo mbalimbali, ikiwemo kuepuka kuvaa mavazi yasiyostahili sehemu za
kazi. Msajili Mkuu huyo wa Mahakama alitoa zawadi ya vazi la skafu kwa baadhi
ya watumishi wa Mahakama hiyo.
Aidha, Mhe.
Chuma aliwahimiza watumishi hao kufuatilia taarifa mbalimbali zilizoko katika
Mpango Mkakati wa Mahakama ili waweze kuufahamu kwa ustandi na kuwa tayari kuutekeleza
kikamilifu.
Alisema
kuwa sanjari ya kuelewa Mpango huo, watumishi wa Mahakama wanapaswa kuendelea kutumia
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kutoa huduma mbalimbali kwa
wananchi.
Aliwataka
watumishi wa Kituo hicho kuhakikisha wanamaliza mashauri kwa wakati na kuepuka
mlundikano kwa kufanyakazi kwa bidii na kwa ufanisi.
Katika
ziara hiyo, Msajili Mkuu huyo alibaini uchakavu, upungufu wa vitendea kazi na
ufinyu wa jengo la Kituo hicho, hali inayolazimu kukosa sehemu ya kuhifadhia majalada
na vielelezo.
Baadhi ya watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Manundu wakiwa wamevaa skafu ambazo walikabidhiwa na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma akiwa katika ziara kwenye Mahakama hiyo.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni