Ijumaa, 28 Oktoba 2022

WADAU MAHAKAMA MOROGORO WAKUBALIANA KESI KUSIKILIZWA MAPEMA

Na Evelina Odemba – Mahakama Morogoro

Mahakama mkoani Morogoro imekubaliana na wadau wake kuanza kusikiliza kesi kuanzia asubuhi ili kuharakisha huduma za utoaji haki kwa wananchi.

Hayo yameazimiwa na wadau wa Mahakama katika kikao cha kusukuma mashauri kilichofanyika leo tarehe 28 Octoba, 2022.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Japhet Manyama, ambaye aliongoza kikao hicho alisisitiza kuwa kesi zitaanza kusikilizwa muda uliopangwa, hivyo kila mdau asimame kwenye nafasi yake.

Aidha, wajumbe katika kikao hicho waliazimia kuwa walaka uliotolewa wa kuwataka mamlaka husika kuleta kesi za jinai mahakamani baada ya upelelezi umekamika uendelee kufuatwa ili kupunguza mrundikano wa watu magerezani.

Kikao cha kusukuma mashauri ambacho huwakutanisha wadau wa Mahakama hufanyika kila baada ya miezi mitatu kufanya kutathmini ya mwenendo wa mashauri na kuweka mikakati ili kuhakikisha utoaji haki unafanyika kwa wakati na kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokea.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Japhet Manyama akichukua kumbukumbu kutoka kwa mdau wakati wa kikao cha kusukuma mashauri (wajumbe hawapo pichani).
Majadiliano yakiendelea katika kikao cha kusukuma mashauri. Aliyekaa katikati ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Japhet Manyama na walioko pembeni yake ni wadau wa Mahakama.
Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Irene Lyatuu (wa kwanza kulia) akitoa mchango wakati wa kikao.

Wadau wakifatilia kikao kwa makini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni