Jumamosi, 24 Desemba 2022

ENDELEENI KUDUMISHA MAADILI MEMA : JAJI LILIAN

 

Na Magreth Kinabo – Mahakama

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Lilian Mashaka amewataka watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kuendelea kufanya kazi kwa kuzingatia maadili mema, bidii, upendo, umoja na ushirikiano ili kuweza kutimiza jukumu la mapambano dhidi ya rushwa.

Akizungumza jana katika hafla ya kuwaaga viongozi waliohama kwa uteuzi, watumishi waliohama na waliostaafu wa Mahakama hiyo, iliyofanyika jana jioni, kwenye  viwanja vya Divisheni hiyo, iliyoko Jijini Dar es Salaam katika Shule ya Sheria alisema amefarijika kuona watumishi hao wakiendelea kufanya kazi kwa kuzingatia vigezo hivyo.

“Dumisheni maadili mema katika utendaji wa kazi sote tunatagemeana katika jukumu kubwa la mapambano dhidi ya rushwa, Divisheni hi inangaliwa kwa jicho la pili, hivyo onesheni ukomavu wa kazi hii.“Sijasikia mkisemwa vibaya ningesikia ningewaambia,” alisema Jaji Lilian.

Aidha Jaji Lilian aliwaambia kwamba maisha mazuri yanakuja kutokana kufanya kazi kwa bidii katika mazingira magumu.

Kwa Upande wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda Bukoba, Mhe. Immaculata Banzi aliongeza kuwa watumishi hao wasifanyekazi kwa kunung’unika, hivyo wafanye kazi kwa nidhamu na kuheshimiana.

Naye Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda alisema watumishi wa divisheni hiyo kuendelea kufanya kazi kwa kuongozwa na roho Mtakatifu katika kutenda haki kwa wananchi.Hivyo anajivunia kuwa watumishi wenye maadili mema na kufanya kazi kwa bidii, ambapo kila mmoja anajipanga katika kazi yake.

Akizungumza kwa niaba ya wastaafu wenzake, Bi. Mchawi Mwanasoro, ambaye alikuwa Mhudumu katika Divisheni hiyo, aliwaomba watumishi hao, kujitahidi kufanya kazi kwa moyo mmoja kswa kuwa ukifanyakazi vizuri itaonekana, ambapo pia aliwaomba kupukana na vitendo viovu.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Lilian Mashaka, (kulia) akipewa zawadi na   Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda ikiwa ni ishara ya kuagwa baada ya kupata uteuzi,  katika hafla ya kuwaaga viongozi waliohama kwa uteuzi, watumishi waliohama na waliostaafu wa Divisheni hiyo, iliyofanyika jana jioni, kwenye  viwanja vya mahakamni hapo , iliyopo Jijini Dar es Salaam katika Shule ya Sheria.


Jaji wa Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda akimlisha  keki   kwa ajili ya kumuaga Bi. Mchawi Mwanansoro, ambaye amestaafu kwa mujibu wa utumishi wa umma katika hafla hiyo.

Jaji wa Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda akimpatia zawadi  Katibu Mustasi Bi. Emmanuela Peter kwa ajili ya kumuaga  baada ya kupangiwa kituo kingine cha kazi.

Watumishi waagwa wakiwa katika hafla hiyo.

 Baadhi ya watumishi wakicheza Bi. Mchawi Mwanasoro,( aliyevaa kitenge) ambaye alikuwa Mhudumu katika Divisheni hiyo.

Jaji Jwa Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda akizungumza jambo kwenye hafla hiyo.Kushoto ni Jaji wa Divisheni  hiyo, Mhe. Godfrey Issaya.


Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Bi. Masalu Kisasila akitoa utambulisho katika hafla hiyo.


 Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Magdalena Ntandu akiongoza sala kwa ajili ya hafla ya kuwaaga viongozi waliohama kwa uteuzi, watumishi waliohama na waliostaafu wa Mahakama hiyo, iliyofanyika jana jioni, kwenye  viwanja vya Divisheni hiyo, iliyoko Jijini Dar es Salaam katika Shule ya Sheria.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda Bukoba, Mhe. Immaculata Banzi (kulia)  akipewa zawadi na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Elinaza Luvanda ikiwa ni ishara kuaagwa baada kupangiwa kituo kingine cha kazi.

Baadhi ya watumishi wa Divisheni hiyo wakicheza na watumishi waagwa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni