Alhamisi, 26 Januari 2023

MAJAJI WA MAHAKAMA YA ARDHI WATOA ELIMU YA USULUHISHI

 

Na Magreth Kinabo-Mahakama

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi. Mhe. Agnes Mgeyekwa leo tarehe 26 Januari, mwaka 2023 amewaongoza majaji wa Mahakama hiyo kutoa elimu ya usuluhishi ili kuweza kutatua migogoro ya ardhi kwa njia hiyo.

Jaji huyo aliambatana na majaji wenzake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa elimu hiyo, na kuweza kuzungumza na baadhi ya wananchi ambapo Wiki ya Sheria inapoadhimishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari, kwa niaba ya majaji wenzake, Jaji wa Mahakana Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi, Mhe. Dkt. Benhaji Masoud alisema   wanatoa elimu hiyo ili kuweza kutatua migogoro ya ardhi kabla ya kufika mahakamani, kwa kuwa hivi sasa migogoro hiyo inafanyiwa usuluhishi baada ya kufika mahakamani.

“Utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa njia hiyo ni unaokoa gharama, muda, kudumisha mahusiano na kukuza uchumi. Hivyo usuluhishi ni njia pekee ya kutatua migogoro ya ardhi,” alisema Jaji Masoud.

Alitoa wito kwa wananchi kutumia njia ya usuluhishi, kwa kuwa ni vigumu kuzaa mgogoro mwingine. Jaji Masoud aliowaomba wananchi kufika katika banda ya Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi ili kuweza kupata uelewa wa utumiaji wa njia hiyo, ikiwa ni hatua ya kuwawezesha kushiriki katika shughuli za uzalishali mali na kukuza uchumi.

Baadhi ya wananachi waliopata elimu hiyo, waliwaomba wananchi wenye migogoro ya ardhi kufika katika banda hilo ili kuweza kuelimishwa njia sahihi ya kutatua suala hilo.

Mahakama hiyo kwa kipindi cha mwaka 2021 ilibakia na mashauri 1,591 mwaka 2022 ilisajili mashauri 2,111 kwa njia ya mtandao, mashauri yaliyoamriwa ni 2,768 sawa na asilimia 131 na yanayoendelea ni 934.

Wiki hiyo ilianza kuadhimishwa Januari 22, mwaka 2023 hadi Januari 29, mwaka 2023 huu yenye kauli mbiu ya “Umuhimu Wa Utatuzi wa Migogoro kwa Njia ya Usuluhishi Katika Kukuza Uchumi Endelevu.”

Kanali Mstaafu Merikiori Mtega (kushoto) akipata elimu kuhusu utumiaji wa njia ya usuluhishi katika kutatua migogoro ya ardhi kutoka kwa mahakama hiyo leo, kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kutoka (kushoto wa pili) ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi. Mhe. Agnes Mgeyekwa, wa (kwanza kushoto) ni mhe. Jaji Dkt.Theodora Mwenegoha. (Kulia wa pili) ni Mhe. Jaji Dkt. Benhaji Masoud na wa kwanza kulia ni Mhe Jaji Kevin Mhina. 


Gratiana Rwakibarila (kushoto) akipata elimu kuhusu utumiaji wa njia ya usuluhishi katika kutatua migogoro ya ardhi kutoka kwa mahakama hiyo leo, kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kutoka (kushoto wa pili) ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Ardhi. Mhe. Agnes Mgeyekwa, wa (kwanza kushoto) ni mhe.Jaji Dkt.Theodora Mwenegoha. (Kulia wa pili) ni Mhe. Jaji Dkt. Benhaji Masoud na wa kwanza kulia ni Mhe Jaji Kevin Mhina.


Hamis Kipande (kulia) na Ismail Omary wakipata elimu kuhusu utumiaji wa njia ya usuluhishi katika kutatua migogoro ya ardhi kutoka kwa mahakama hiyo leo, kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.  (wa kwanza kushoto) ni mhe. Jaji Dkt.Theodora Mwenegoha. (katikati) ni Mhe. Jaji Dkt. Benhaji Masoud na kulia ni Mhe Jaji Kevin Mhina.

 

  

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni