Na. Ahmed Mbilinyi – Mahakama, Bukoba
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Bukoba, Mhe. Immaculate Banzi leo tarehe 21 Februari,
2023 amefanya ziara ya ukaguzi katika Mahakama ya Wilaya Kyerwa mkoani Kagera.
Akizungumza katika ziara
hiyo, Mhe. Banzi alisisitiza watumishi kufanya kazi kwa ushirikiano na
kuzingatia maadili na nidhamu ili kufanikisha malengo ya Kanda pamoja na kuboresha
huduma za utoaji haki kwa wananchi.
Jaji Mfawidhi huyo amesisitiza
kuwa ni muhimu kwa watumishi wa Mahakama hiyo kutoa huduma nzuri kwa wananchi na
kulitunza jengo hilo.
Itakumbukwa jengo la Mahakama
ya Wilaya Kyerwa ni mojawapo ya majengo mapya 18 yaliyozinduliwa na Jaji Mkuu
wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma tarehe 25 Novemba, 2022. Uzinduzi wa
majengo hayo ulifanyika katika Mahakama ya Wilaya Busenga mkoani Simiyu.
Viongozi wengine
waliokuwapo katika ziara hiyo ya ukaguzi ni pamoja na Msajili wa Mahakama Kuu
Kanda ya Bukoba, Mhe Amworo Odira, Mtendaji wa Mahakama kutoka Kanda hiyo, Bw.
Lothan Simkoko, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kyerwa, Mhe.
Flavian Kubigwa pamoja na Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo katika Wilaya ya
Kyerwa na watumishi wengine.
Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Bukoba, Mhe. Immaculata Banzi (aliyeketi
katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama pamoja na
watumishi wa Mahakama ya Wilaya Kyerwa. Wengine walioketi kuanzia kulia ni Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kyerwa, Mhe. Flavian Kubigwa, Msajili wa Mahakama
Kuu Kanda ya Bukoba, Mhe. Oodira Amworo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya
Bukoba, Bw. Lothan Simkoko na Afisa Tawala Mahakama ya Wilaya Kyerwa, Bw.
Prudence Bitumbi.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni