Jumamosi, 25 Februari 2023

TANZIA; MTUMISHI WA MAHAKAMA YA MWANZO NYAMBONO AFARIKI DUNIA

Marehemu Nicolaus Mgeta Rumbe enzi za uhai wake.

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake   Bw. Nicolaus Mgeta Rumbe (katika picha) aliyekuwa Mtumishi wa Mahakama ya Mwanzo Nyambono iliyoko Wilayani Musoma.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, Bw. Festo Chonya marehemu Rumbe alifikwa na umauti  tarehe 23/02/2023 kutokana na ugonjwa wa kisukari.

 Mazishi yake yamefanyika leo tarehe 25/02/2023 katika kijiji cha Bugoji kilichopo Musoma Vijijini.

Marehemu Nicolaus Mgeta Rumbe alizaliwa 12/07/1966 na kuajiriwa katika Mahakama ya Tanzania tarehe 16/04/1984.

Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki kuomboleza katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wetu.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni