Na Eva Leshange- Mahakama, Singida
Mahakama Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Dodoma imepanga kushughulikia mashauri yanayohusu mauaji 17 katika
kipindi cha mwezi mmoja.
Naibu Msajili wa Mahakama
Kuu kutoka Kanda hiyo, Mhe. Silivia Lushasi amesema mashauri hayo yatasikilizwa
na Majaji wawili kwenye vikao maalumu (sessions) vinavyofanyika mkoani Singida.
Majaji hao kutoka
Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma ni Mhe. Suleiman Hassan ambaye atasikiliza mashauri tisa kuanzia tarehe 13 Februari, 2023 hadi
tarehe 28 Februari, 2023.
Jaji mwingine ni Mhe. Fatma Khalfan ambaye atasikiliza mashauri nane na
ataanza jukumu hilo tarehe 1 Machi, 2023 hadi tarehe 16 Machi, 2023.
“Sambamba na taarifa hii, Mkoa wa Singida una
mashauri 16 ambayo yanasubiri kusikilizwa (uncauselisted) ambapo Mahakama ya Hakimu
Mkazi kuna mashauri 10, Iramba manne na Manyoni mawili,” Naibu Msajili huyo
alisema.
Mhe. Lushasi alibainisha
kuwa idadi hiyo ya mashauri tajwa haihusishi mashauri yanayosubiri washitakiwa
kusomewa kwa mara ya kwanza (plea taking). Katika kikao hicho wadau wameahidi
kutoa ushirikiano mkubwa na wamejipanga vizuri ili kuhakikisha mashauri hayo
yanamalizika.
Sehemu ya wajumbe wa kikao wakifuatilia kwa umakini mjadala.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni