Alhamisi, 2 Machi 2023

JAJI KIONGOZI KUFUNGA KIKAO KAZI CHA MAPITIO YA BAJETI KESHO

 

Na Magreth Kinabo-Mahakama

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani kesho tarehe 3 Machi, 2023 anatarajiwa kufunga kikao kazi cha cha mapitio ya bajeti ya nusu ya mwaka 2022/23 na uchambuzi wa  maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24  ya Mahakama ya Tanzania.

Kikao hicho kilianza tarehe tarehe 27 Februari 2023 kinachoendelea Jijini Dodoma, ambapo lengo lake ni  kufanya mapitio ya kina ya utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha nusu  ya kwanza ya mwaka 2022/23 na kuchambua mipango  ya  maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023 /24  ya Mahakama hiyo.

Akizungumzia kuhusu kikao hicho, Mkurugenzi wa Mipango na Ufuatiliaji, Bw.Erasmus Uisso alisema  kinaenda vizuri na kinamalizika leo tarehe 2 Machi, 2023 kwa mujibu wa ratiba. Hivyo kila kanda ya Mahakama na Divisheni imejiandaa vizuri.

‘‘Katika kikao hiki kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2023/24 eneo la usikilizaji wa mashauri limepewa kipaumbele ili liweze kuwa na bajeti ya kutosha,’’ alisema Uisso.

Aliongeza kwamba kupitia maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24 kanda za Mahakama zimewasilisha mahitaji ya nyongeza kwa sababu ya uanzishaji wa mahakama za wilaya mpya na uanzishaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara. Pia alisema mahitaji bajeti ya nyongeza imetokana na mpango wa kuanzisha Mahakama Kuu Kanda ya Geita inayotajiwa kuanza  kufanya kazi Julai, mwaka 2023.

Mkurugenzi huyo aliishukuru Serikali kwa mgawo wa fedha ambao iliutoa kwa kila ngazi ya Mahakama kama ilivyopangwa kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali.

Aidha Uisso alisema bado Mahakama hiyo inakabiliwa na changamoto ya mahitaji ya vitendea kazi, magari,kompyuta na uhaba wa watumishi.

Mwenyekiti wa  kikao kazi cha mapitio ya bajeti ya nusu mwaka 202/23 na uchambuzi wa maandalizi ya  bajeti ya mwaka 2023/24 ya Kituo Jumuishi cha Masuala ya Kifamilia,Bw.Leonard Magacha akiongoza kikao hicho leo kinachoendelea Jijini Dodoma.

Mjumbe wa kikao hicho, Mhe. Sharmillah Sarwatt (kulia) akizungumza jambo kuhusu bajeti hiyo. Anayefuatia ni mjumbe wa kikao hicho, Bw.Joseph Elikana.

Mtendaji wa ya Kituo Jumuishi cha Masuala ya Kifamilia, Bi. Mary Shirima wa (pili kushoto) akifafanua jambo kwenye kikao hicho, wengine (wa mwisho kushoto)ni Naibu Msajili wa kituo hicho Mhe. Martha Mpaze na watatu kutoka kushoto ni Leornard Kilala ambaye ni Afisa Tawala na (kwanza kushoto) ni Mkaguzi wa Ndani,Bw, Mujaya Mujaya  wote kutoka kituo hicho.


Wajumbe kutoka Mahakama Kuu ya Tabora (walioketi kulia) wakiwasilisha  mapitio ya bajeti yao, na walioketi (kushoto katikati) ni jopo la kikao hicho likiongozwa na Mwenyekiti wa kikao kazi hicho Godfrey Mashafi, (aliyeketi katikati mbele)ni Katibu wa jopo hilo, Bi. Zawadi   Ngonde.

Wajumbe wa kikao hicho kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya wakiwasilisha mapitio ya bajeti yao wa (kwanza kushoto mwenye shati la damu ya mzee)ni Mtendaji wa Kanda hiyo Bw. Teofard Ndomba(katikati) ni Naibu Masajili wa Kanda hiyo, Mhe. Projesta Kahyoza na (tatu kushoto)ni Afisa Bajeti, Bw.Joseph Namiata.

Mwenyekiti wa Kikao hicho cha bajeti ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Dkt. Angelo Rumisha  akizungumza jambo na (kulia) ni mjumbe wa kikao hicho, Mhe. Kinabo Minja akifuatilia  mapitio ya bajeti ya kanda hiyo.

Wajumbe wa kikao hicho kutoka Mahakama wakiendelea kuhitimisha kazi hiyo.

 

 

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni