Jumanne, 7 Machi 2023

TAWJA KIBAHA YATEMBELEA KITUO CHA AFYA MKOANI PWANI

Na Eunice Lugiana-Mahakama, Kibaha

Katika kuelekea siku ya wanawake duniani, Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, kupitia wawakilishi wake hivi karibuni walitoka elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kifamilia katika wodi ya wazazi kwenye Kituo cha Afya Mkoani.

Akiongea na wazazi wanasubiria kujifungua wapatao kumi na mbili (12) kuhusu ukatili, mwakilishi huyo ambaye ni Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Mailimoja, Mhe. Rosely Mwakila alisema vitendo vya kudharauliwa, kukeketwa pamoja na ubakaji ni ukatili wa kijinsia.

Aliwaomba wazazi hao endapo wakiona viashiria vya vitendo hivyo watoe taarifa kwenye vyombo husika, ikiwemo Serikali za Mtaa, Ofisi ya Kata, ustawi wa jamii au Dawati la Jinsia Polisi.

Wakati huo huo, wito umetolewa kwa wazazi kuandika majina halisi ya baba wa mtoto pindi wanapojifungua ili kuepuka usumbufu endapo baba mzazi wa mtoto akifariki.

Wito huo umetolewa na Mwakilishi wa TAWJA Wilaya ya Kibaha, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Mailimoja, Mhe. Honorina Kambadu, wakati akiwa katika wodi wa wazazi waliojifungua kwa njia ya kawaida katika kituo hicho.

Aidha, Mhe. Kambadu amesema wapo wanawake wanaozaa na wanaume wenye familia na kumficha mtoto ili alisifahamiane na zake na pia kumpa jina  ambalo sio la baba yake mzazi, hivyo kumnyima haki ya kurithi endapo baba atafariki.

Mwakilishi wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJAa) Mhe. Honorina Kambadu (kulia) na viongozi wengine wakiwa katikia Kituo cha Afya Mkoani.

Wanawake kutoka maeneo mbalimbali waliohudhuria kliniki katika Kituo hicho.

Madaktari na Manesi wa Kituo cha Afya Mkoani wakisikiliza utoaji wa elimu.

 (Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni