Ijumaa, 3 Machi 2023

WANAOKWAMISHA MABADILIKO YA MAHAKAMA KUCHUKULIWA HATUA

 

Na Magreth Kinabo na Stanslaus Makendi Mahakama, Dodoma

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani amesema kwamba uongozi wa Mahakama ya Tanzania utachukua hatua ya kumwajibisha mtumishi yoyote yule ambaye atakuwa ni kikwazo wa mabadiliko  yanayofanywa na mhimili huo katika kuelekea safari ya Mahakama Mtandao ifikapo mwaka 2025.

Aidha, Jaji Kiongozi amewataka Watendaji wa Mahakama mbalimbali kutosita kuwachukulia hatua watumishi wazembe waliochini yao.

Mhe.  Siyani alizungumza hayo leo   tarehe 3 Machi, 2023 wakati akifunga kikao kazi cha mapitio ya bajeti ya nusu ya mwaka 2022/23 na uchambuzi wa maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24  ya Mahakama kilichofanyika Jijini Dodoma, ambapo alisitiza ushirikiano wa utendaji kazi kwa watumishi hao.

‘‘Hakuna mabadiliko yanaweza kutokea bila uwajibikaji. Kila mmoja wenu ni lazima atimize wajibu wake kwa vitendo ili kuhakikisha anatimiza jukumu muhimu la suala la utoaji haki iliyobora kwa usawa na wakati na kuendana na mabadiliko hayo,’’ alisema Jaji Kiongozi.

Aidha Jaji Siyani aliwataka kushirikiana katika utendaji kazi na kila mmoja kujiuliza kuwa anaisadiaje Mahakama ya Tanzania katika kusonga mbele na kupata mafanikio ikiwemo kuondoa fikra kila kitu kitafanywa na Makao Makuu.

‘‘Kila mtu awajibike kwa nafasi yake mnapopanga bajeti vipaumbele viwe ni vya taasisi.’’ alisisitiza.

Aliwataka Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama mbalimbali kushirikiana katika kufanikisha mabadiliko hayo. kwa kuwa mafanikio yatapatikana kutokana na nafasi ya kila mmoja.

Mhe. Siyani aliongeza kuwa huu ni mwaka wa kufanya mabadiliko ya kutoa huduma bora, hivyo kila mtu awajibike kwa hilo. Aliongeza kuwa watumishi hao wanatakiwa kuwa wabunifu ,ikiwemo umiliki wa mabadiliko hayo. Pia wanapaswa kufahamu utamaduni wa Mahakama.

Kwa upande mwingine, Jaji Kiongozi aliwataka wajumbe wa kikao kazi hicho, kuangalia vyema namna wanavyopanga bajeti za maeneo yao na kuona ni kwa jinsi gani wanaweza kuzisaidia Mahakama za Mwanzo kwa kuwa asilimia 70 ya mashauri yanatoka katika Mahakama hizo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Viongozi wa Menejimenti ya Mahakama, Naibu Wasajili, Watendaji wa Mahakama, Mahakimu Wakazi Wafawidhi na Maafisa Bajeti kutoka Mahakama  mbalimbali nchini.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani akitoa hotuba yake  leo   tarehe 3 Machi, 2023 wakati akifunga kikao kazi cha mapitio ya bajeti ya nusu ya mwaka 2022/23 na uchambuzi wa maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24  cha Mahakama ya Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma.

Wajumbe wa Menejimenti ya Mahakama ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja kwenye kikao hicho.

Baadhi ya wajumbe  wakiwa katika kikao hicho, wakimsikiliza Jaji Kiongozi.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma akisisitiza jambo kwenye kikao hicho.

Sehemu ya wajumbe  wakiwa katika kikao hicho (Juu na chini), wakimsikiliza Jaji Kiongozi.


Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Bajeti wa  Mahakama mbalimbali nchini. Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (kushoto) na (kulia) ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma. 

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama mbalimbali nchini. Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (kushoto)na kuliani Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya kikao hicho. Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (kushoto)na kuliani Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Wasajili mbalimbali nchini. Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (kushoto)na kuliani Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma. 

(Picha na Mahakama ya Tanzania).



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni