Alhamisi, 9 Machi 2023

WANAWAKE MAHAKAMA KIGOMA WASHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Na Aidan Robert-Mahakama, Kigoma

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Rose Kangwa ameongoza wanawake wa Mahakama katika Kanda ya Kigoma kusherekea siku ya mwanamke duniani.

Kwa Mkoa wa Kigoma sherehe hiyo imefanyika katika Kata ya Kidahwe, Wilaya ya Kigoma. Akizungumza katika hafla hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Mhe. Lameck Mlacha amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake ni nyenzo muhimu kuiwezesha Kanda hiyo kuwa kinara katika utendaji kazi.

Kauli mbiu ya maadhimishio hayo inasema Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia:Chachu katika kuleta Usawa wa Kijinsia. Alisema siku hiyo iwe chachu ya maendeleo na kuwainua wanawake kiuchumi na kielimu ili kujenga uchumi endelevu wa nchi.

Mhe. Mlacha alibainisha kuwa maendeleo ya teknolojia yakawabadilishe wengi ili watumie muda mwingi kujijengea uwezo wa kufanya kazi na maendeleo binafsi ya kiuchumi ili kuwa na maendeleo bora ya familiya na uchumi wa nchi katika kuongeza ubunifu wa mambo mbalimbali mahali pakazi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Mhe. Lameck Mlacha (katikati) akisisitiza jambo katika hafla hiyo. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu kutoka Kanda hiyo, Mhe. Stephan Magoiga (kushoto) na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mhe. Rose Kangwa (kulia).
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mhe. Rose Kangwa (wa kulia) na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya Kigoma, Mhe. Eva Mushi wakiongoza maandamano ya wanawake katika Siku ya Wanawake duniani.
Baadhi ya wanawake wa Mahakama Kanda ya Kigoma waliojitokeza katika sherehe hiyo.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Mwandiga, Mhe. Florence Ikolongo akiwa ameshika bango lililobeba kauli mbiu ya siku ya mwanawake duniani. Kushoto kwake ni Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi, Mhe. Anna Kahungu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma, Mhe. Lameck Mlacha (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanawake waliojitokeza kwenye sherehe hiyo.

(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni