Jumanne, 2 Mei 2023

WANACHAMA WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU SINGIDA WAKUTANA

Na Eva Leshange-Mahakama Singida

Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) Tawi la Singida hivi karibuni kilikutana kujadili masuala mbalimbali ya kazi na kupeana mbinu za kuinuana kiuchumi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Singida, Mhe. Allu Nzowa ndiye aliyefungua Kikao hicho ambacho kilichofanyika katika Wilaya ya Manyoni.

Kufanyika kwa Kikao hicho ni muendelezo wa vikao ambavyo wanachama wa JMAT wamekuwa wakifanya mara kwa mara ili kujengeana uwezo na kujadili masuala ambayo Mahakimu hukutana nayo katika vituo vyao vya kazi, kutatua changamoto na kupeana uzoefu na mbinu mbalimbali za stadi za maisha.

Vikao hivyo vimekuwa na tija hasa kwa Mahakimu wageni kwani wanapata fursa ya kujifunza mambo yanayohusu tasnia kwa undani na kwa vitendo zaidi na pia vimekuwa msaada ambapo hukumbushana sheria mbalimbali na mabadiliko yake.

Katika kikao hicho, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela, katika mada ya kupeana uzoefu aliwasisitiza Mahakimu kutojifungia ndani badala yake wajishughulishe na shughuli nyinginezo za kujipatia kipato na kutokutegemea mishahara pekee.

“Waheshimiwa wenzangu tusijifungie ndani, tujiongeze kwa kufanya shughuli nyinginezo zitakazotuongezea kipato ili kuboresha na kupunguza ukali wa maisha,” alisema.

Vile vile aliwapa uzoefu alionao katika shughuli za ufugaji wa kuku, kilimo na biashara ya mazao na mifugo.Wajumbe wengine walitoa uzoefu katika biashara mbalimbali.

Baada ya kupeana uzoefu wa kazi na mbinu za kuinuana kiuchumi ulifanyika uchaguzi wa Mwenyekiti wa JMAT Tawi la Singida baada ya Mwenyekiti aliyekuwepo awali kuhama Mkoa na Mhe. Esther Mpanga alishinda kwa kishindo.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa akzungumza wakati anafungua kikao kazi cha wanachama wa Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) Tawi la Singida.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu. Wengine waliokaa ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Manyoni, Mhe. Alisile Mwankejela(kushoto), Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Iramba,  Mhe. Christopher Makwaya (wa pili kushoto), Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Manyoni Mjini, ambaye pia ni Katibu wa JMAT Tawil la Singida,  Mhe. Gidion Kilaga na Mtendaji wa Mahakama Singida, Bw. Yusuph Kasuka.

Meza Kuu ikiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (katikati waliokaa) ikiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya Singida.

Meza Kuu ikiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (katikati waliokaa) ikiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu wa Wilaya ya Manyoni.

Meza Kuu ikiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama Hakimu Mkazi Singida, Mhe. Allu Nzowa (katikati waliokaa) ikiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu wa Wilaya ya Iramba.

(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni