Jumatano, 31 Mei 2023

WATUMISHI MAHAKAMA MBEYA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU AFYA YA AKILI

Na Mwinga Mpoli, Mahakama Kuu Mbeya

Watumishi wa Mahakama Mkoa wa Mbeya wamepatiwa mafunzo ya afya ya akili ili kuboresha huduma wanazotoa kwa wateja kwa makundi yote.

Mafunzo hayo yalizinduliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dastan Ndunguru hivi karibuni ambayo yalifanyika katika ukumbi wa Mahakama hiyo.

“Matatizo ya afya ya akili hayachagui, mtu yeyote anaweza kuyapata. Sisi kama taasisi tunafaidika na mafunzo haya kwa sababu afya ya akili ni kila kitu. Tukijiangalia hapa tunajiona tuna akili, lakini tukipimwa tunaweza kujikuta wote tuna matatizo,” alieleza.

Kwa upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu Mbeya ambae ni mratibu wa mafunzo, Mhe. David Ngunyale alisema kuwa kutokuwa na utulivu wa kiakili kunaweza kuathiri familia, mwajiri, wananchi na nafsi pia, hivyo ni vema kuwa na mafunzo hayo ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Jaji mwingine anayehudumu katika Mahakama hiyo, Mhe. Victoria Nongwa, akizungumza wakati ana ahirisha mafunzo hayo alisisitiza watu kujipenda na kupunguza matarijio makubwa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dastan Ndunguru akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo.
Msaikolojia, Bi Betuna Mwamboneke akieleza jambo.

Majaji wa Mahakama Kuu Mbeya na viongozi wengine waandamizi wakiwa katika mafunzo hayo.

Watumishi wa Mahakama Mbeya (juu na chini) wakifuatilia mafunzo.


(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni