Na Evelina Odemba- Mahakama, Morogoro
Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, imemuachia huru bila masharti yeyote Askari
wa Jeshi la Polisi mwenye Namba G.88808 Koplo Mapalala aliyekuwa anakabiliwa na
shtaka la kuuwa bila kukusudia.
Hukumu
hiyo ilitolewa na Jaji Messe Chaba hivi karibuni baada ya kusikiliza ushahidi
uliowasilishwa na upande wa mashtaka na utetezi. Katika shauri hilo, Jamhuri iliwakilishwa
na Wakili wa Serikali Elias Masini wakati upande wa utetezi ukiwakilishwa na
Wakili Msomi Fredy Sanga.
Koplo
Mapalala alikabiliwa na shtaka la kumuua Hamis Mng’ombe (30), Mkazi wa Mvua, tarehe
31 Mei, 2022 katika mazingira yaliyopelekea kutumia risasi za moto ili
kuwatawanya wananchi wenye hasira kali waliokuwa wamemzunguka.
Akisoma
hukumu ya shauri hilo, Mhe. Chaba alizingatia shufaa zilizowasilishwa na upande
wa utetezi kuwa mshitakiwa alikuwa kwenye kutekeleza majukumu yake ya kazi
ambapo alijikuta amezingirwa na kundi la watu wenye silaha za jadi wakiwa na
lengo la kumzuru.
Mhe.
Chaba alieleza kuwa wakati akijitetea kulinda silaha na kuutetea uhai wake Askali
huyo alifyatua risasi iliyompata marehemu kwenye mguu na kusababisha jeraha
lililopelekea kifo chake baada ya kuvuja damu nyingi.
Hata
hivyo, alitoa onyo kuwa kalamu ya Askali ni bunduki, hivyo wanapaswa kuitumia
vizuri kuleta amani sehemu yenye uvunjifu wa amani na sio kuitumia kukatisha
uhai.
Akizungumza
mara baada ya hukumu hiyo kutolewa, Wakili Sanga alisema kuwa wamepokea kwa
furaha uamuzi huo na kuipongeza Mahakama kwa maboresho makubwa iliyoyafanya
kwakuwa imeweza kusikiliza kesi hiyo ndani ya mwaka mmoja.
“Tunafurahishwa
na maboresho yanayofanywa na Mhimili wa Mahakama, kesi hii imechukua mwaka
mmoja tu, jambo ambalo miaka mitatu nyuma lilikuwa ndoto,” alisema.
Alibainisha
kuwa hapo awali walikuwa wanategemewa Majaji kutoka Dar es Salaam wapangiwe kikao
maalumu ndipo waje kusikiliza, lakini kwa sasa tunashuhudia shauri
limesikilizwa na Jaji wa hapa, kwa kweli Mahakama inafanya vizuri,” alieleza.
Kesi zingine 11 zitasikilizwa katika kikao hiki mbele ya Mhe. Chaba aliyeanza tarehe 28 Agosti,2023 na anategemea kuhitimisha tarehe 22 Septemba, 2023.
Jaji
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Messe Chaba.
Jengo
la Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni