Jumanne, 26 Septemba 2023

JAJI MFAWIDHI SONGEA AMTEMBELEA MKUU WA MKOA RUVUMA

Na Hasani Haufi- Mahakama Songea

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha hivi karibuni alimtembelea Mkuu wa MKoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas kwa ajili ya kumsalimia na kujitambulisha.

Mkuu wa Mkoa alionyesha kufurahishwa na kitendo hicho na kuahidi kumpa ushirikiano ili aweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu kwani imekuwa desturi kwa Viongozi wa Mahakama kumtembelea pindi wanapofika mkoani Ruvuma.

Kanali Thomas alimweleza Jaji Mfawidhi kuwa maadili ya watumishi wa Mahakama yameimarika kwani malalamiko kutoka kwa wananchi yamepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na uelewa wa huduma zinazotolewa mahakakani.

“Kupitia elimu zinazotolewa kila siku na Mahakama Kanda ya Songea na pia kupitia vyombo vya habari, wananchi wamekuwa na uelewa wa kutosha kuhusu huduma zinazotolewa na wanajuwa mambo mengi kupitia jukwaa hili,” amesema.

Mkuu wa Mkoa alimwomba Jaji Mfawidhi kudumisha mahusiano mazuri yaliyopo kwani ushirikiano wa mihimili yote ya dola unasaidia kuimarisha utendaji, hivyo kuongeza imani ya wanachi ambao ndiyo wanufaika wakubwa wa huduma zinazotolewa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa Kanali Laban Thomas.

Picha ya pamoja kati ya Jaji Mfawidhi (kulia) na Mkuu wa Mkoa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas (wa tatu kushoto) pamoja na Viongozi wengine wa Mahakama.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha(mwenye miwani) akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas.

(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni