Jumatatu, 4 Septemba 2023

MAHAKAMA SONGWE YAENDELEA KUTOA ELIMU CLUB ZA WANAFUNZI.

Na. Mohamed Kimungu- Mahakama Songwe

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Songwe kupitia kamati ya Elimu Mkoa imewatembelea wanachama wa club ya Mahakama katika shule ya sekondari Ilolo kwa lengo la kutoa elimu kwa wanafunzi hao.

Akitoa elimu kwa wanaclub hao, Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe alisema, kwamba ni jukumu la Mahakama kutoa elimu kwa wanachama wa Club hiyo, kuilea, kuijengea uwezo na kuitembelea kadri ya ratiba ilivyopangwa na Mahakama.

“Ni wajibu wa kila mwanaclub kuhakikisha anatimiza ndoto yake hivyo club hii itumike kama chachu ya kuendelea kuwajengea uwezo kimasomo na kuendelea kujiimarisha ili siku moja mfaidi matunda ya hiki kitu mnachokifanya leo”, aliongeza Mhe. Changwe

Wanafunzi hao wamefurahishwa na elimu kuhusiana na sheria za Mirathi na Wosia iliyotolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Mlowo Mhe. Mesia Gan’golo na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Vwawa Mhe. Martha Malima.

Aidha, akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Mwanafunzi Faraja Chilembe wa kidato cha tatu katika shule hiyo aliupongeza Uongozi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe  kwa jitihada kubwa za kuanzisha club shuleni hapo na kuendelea kutoa elimu ya sheria “napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza Mahakama ya Tanzania kwa kuendelea kuwatembelea na kutoa elimu ya sheria kupitia club yetu tumefarijika kupata elimu ya wosia na mirathi itatusaidia katika maisha yetu ya kila siku”, aliongeza Mwanafunzi huyo.

Akihitimisha zoezi hilo la utoaji elimu kwa Club ya Mahakama iliyopo Shule ya Sekondari Ilolo, Mwenyekiti wa kamati ya Elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe aliwakabidhi wanafunzi hao zawadi ya kalamu boksi nne (4) na kuwataka kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo la utoaji wa elimu na kuwa mabalozi wema ili kufikisha elimu hiyo kwa familia zao na jamii inayowazunguka.

Hakimu Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima akitoa Elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ilolo mkoani Songwe kushoto ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe.


Wanafunzi wa shule ya sekondari Ilolo wakimsikiliza kwa makini mtoa mada wa elimu ya sheria kuhusu wosia na Mirathi inayotolewa shuleni hapo.


Hakimu Mkazi Mahakama ya mwanzo Mlowo Mhe. Mesia Gan'golo (kulia) akitoa elimu kwa wanafunzi wa club ya Mahakama (hawapo pichani), wengine ni  Hakimu Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima (kushoto) na katikati ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe.

Wanafunzi wa shule ya sekondari Ilolo wakimsikiliza kwa makini mtoa mada wa elimu ya sheria kuhusu wosia na Mirathi inayotolewa shuleni hapo.

Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe akifafanua jambo mbele ya wanafunzi wa club hiyo (hawapo pichani), wengine ni Hakimu Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima (kushoto) na Hakimu Mkazi Mahakama ya mwanzo Mlowo Mhe. Mesia Gan'golo (kulia).

Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe akimkabidhi wanafunzi Faraja Chilembe zawadi ya kalamu boksi nne (4) kwa niaba ya wanaclub na kuwataka kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.

Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Mbozi na Mwenyekiti wa kamati ya elimu Mkoa wa Songwe, Mhe. Vitalis Changwe (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi Faraja Chilembe aliyeshika zawadi ya kalamu boksi nne (4) kwa niaba ya wanaclub, Wengine ni Mwalimu Mlezi wa Club Bi. Rehema Msola (wa kwanza Kulia), Hakimu Mahakama ya Mwanzo Vwawa mjini Mhe. Martha Malima (kushoto) na Hakimu Mkazi Mahakama ya mwanzo Mlowo Mhe. Mesia Gan'golo (wa pili kulia).

Habari hii imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni