Jumamosi, 30 Septemba 2023

MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI MOSHI YAFANYA KIKAO KAZI CHA TATHIMINI

Na. Paul Paschal – Mahakama, Moshi

Uongozi na Watumishi wa Mahakma ya Hakimu Mkazi Moshi wamekutana na kufanya kikao kazi cha mapitio ya kiutendaji ya mwezi septemba wenye lengo la kuainisha mafanikio, changamoto na namna ya kuboresha utoaji huduma za kimahakama kwa wananchi na wadau.

Akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika tarehe 29 Septemba, 2023 Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi Mhe. Salome Mshasha alisema,  aliwakumbusha Watumishi wote kutambua dira ya Mahakama  ni moja tu kutoa  haki kwa wananchi  wote na kwa wakati, hivyo ni vyema  katumia maarifa na weledi kufanikisha hilo ni lazima kusimamia misingi ya maadili, nidhamu na uwajibikaji.

Naye Afisa Tawala wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi Bw. Paul Mushi alisema, Watumishi wanapaswa kutunza na kusimamia rasilimali za ofisi ili kuwezesha kutimiza malengo ya ofisi.

“tukiweza kuzimamia rasilimali za ofisi yetu mambo yatakuwa mzauri na kuondoa changamoto. Pia niwaombe kuongeza jitihada katika matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHEMA), vile vile tuhahikikishe taarifa za mashauri yote katika kituo chetu zinauhishwa kwa wakati ili tuwe na taarifa sahihi za kiutendaji”. aliongeza Afisa Tawala huyo. 

Kwa upande wake mtumishi wa Mahakama hiyo, Bw. Robert Cornel alisema, swala la kutoa lugha nzuri kwa mtumishi anapo muhudumia mteja ni la msingi sana katika utoaji haki, hii inajenga faraja kwa wateja hata pale ambapo maamuzi yanakuwa  hayajatolewa kwa upande wake na lugha nzuri daima inapunguza malalamiko.

Kikao hicho hufanyika kila mwisho wa mwezi kwa lengo la kufungua tathimini ya kiutendaji wa shughuli za Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi sambamba na kuweka mipango kwa mwezi unafuata.

Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi Mhe. Salome Mshasha akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha mwezi Septemba cha tathimini kwa watumishi wa Mahakama hiyo (hawapo pichani).


Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi wakifuatilia agenda za kikao kazi hicho cha tathimini cha mwezi Septemba.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni