Na Eunice Lugiana-Mahakama, Kibaha
Wanachama wa Club ya Mahakama
katika Shule ya Sekondari Gili iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani wamefunguka kuuliza
maswali mengi na kutaka kujua hatua muhimu za kuwafanya wawe wanasheria au
Mahakimu.
Hamu ya kufikia hatua hiyo
ilikuja baada ya wanafunzi hao kupata histori ya Hakimu Mkazi Mahakama ya
Wilaya Kibaha, Mhe. Fahamu Kibona aliyowaeleza alipokuwa anatoa elimu ya sheria
katika club hiyo.
Akisimulia historia
yake, Mhe. Kibona alisema wakati yuko kidato cha pili siku moja usiku akiwa
anasoma kwa mtindo wa kuweka miguu kwenye beseni la maji ili asisinzie alisikia
kishindo cha mtu anaruka uzio.
Anaeleza kuwa alipoinuka
alikuta ni mwizi, akamkamata na kumpeleka polisi, baadaye aliitwa mahakamani
kutoa ushahidi wa namna alivyomuona mwizi huyu.
Mhe. Kibona alisema
baada tu ya kufika mahakamani alimuona Hakimu amevaa suti nyeusi ameketi katika
kiti anaendesha kesi, alivutiwa namna anavyouliza maswali.
Alieleza kuvutiwa na
kazi hiyo, hivyo akafuatilia namna gani anaweza kuwa Hakimu na mpaka leo ndoto
yake imetimi na anajivunia kuwa miongoni wa watu wanaotoa haki katika jamii.
Baada ya simulizi hiyo, wanafunzi
katika shule hiyo walijawa na shauku na kutaka kujua zaidi vigezo vunabvyotumika
mpaka mtu kufikia kuwa mwanasheri au Hakimu.Wanafunzi hao walitaka pia kujua
tofauti iliyopo kati ya Hakimu na mwanasheria.
Elimu katika Club ya
Mahakama kwenye Shule ya Sekondari Gili hufanyika kila mwezi. Utoaji wa elimu
hii ya kisheria ilizindiliwa mwezi wa saba mwaka huu.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni