Na Evelina Odemba – Mahakama, Morogoro
Kufuatia kuanzishwa kwa Kituo
cha Huduma Bora kwa mteja katika Mahakama ya Tanzania, watumishi na wateja wa mahakama
katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki wamepatiwa elimu ya namna ya kupata
huduma kupitia kituo hicho.
Elimu hiyo ilitolewa na
wataalamu toka ndani ya kituo hicho, Mahakimu Wakazi Waandamizi, Mhe. Lilian
Silayo na Mhe. Adelf Sachore, ambao walitoa elimu na kuzungumza na wateja wa Mahakama
kwa siku mbili kuanzia jana terehe 10 Oktoba, 2023.
Akitoa elimu hiyo, Mhe. Sachore
alisema kuwa kituo chao ni sehemu ya mpango mkakati wa maboresho ya Mahakama na
Mahakama hukitumia kujitathmini na kufanya maboresho kutokana na maoni
yanayotolewa na wadau wa Mahakama.
“Naomba niwatoe wasiwasi,
kuna usiri mkubwa baina ya mteja na mtu anayempatia huduma, hivyo msisite
kuwasiliana na huduma yetu kwa kuhofia kuwa tutavujisha siri,” alisema na kubainisha
kuwa kituo kitampatia mteja majibu kwa ufasaha mara baada ya suala lake
kushughulikiwa.
Naye Mhe. Silayo akigusia
namna mteja anavyoweza kuwasiliana na huduma ya kituo hicho kwa kutimia simu,
tovuti na ujumbe wa WhatsApp. Alitaja mawasiliano hayo kama namba ya simu 0752 500
400 na tovuti maoni@judiciary.go.tz.
Kwa upande wake, Naibu Msajili
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Agustina Mmbando aliwasihi
wateja hao kutokaa na malalamiko bali walitumie dawati lililoko ndani ya jengo
la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Morogoro ili yatapatiwe ufumbuzi.
Tangu kuanzishwa kwa kituo cha huduma kwa mteja mnamo tarehe 1 Machi, 2022, kimeweza kupokea maoni na malalamiko 2,751 hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Septemba, 2023. Kati ya hayo, 2,740 yametatuliwa na 11 yaliyobaki yanaendelea kufanyiwa kazi.
Mhe. Adelf Sachore kutoka
Kituo cha Huduma Bora kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania akizungumza na wateja
ndani ya Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Morogoro wakati akitoa elimu juu ya
huduma kwa mteja.
Mhe. Lilian Silayo kutoka
Kituo cha Huduma Bora kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania akizungumza na wateja
ndani ya Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Morogoro wakati akitoa elimu juu ya
huduma kwa mteja.
Naibu Msajili wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Agustina Mmbando akizungumza na wateja
wakati wa zoezi hilo la utoaji elimu.
Wateja wakifuatilia elimu
ikiendelea kutolewa (juu na chini).
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni