Jumatano, 11 Oktoba 2023

JAJI MFAWIDHI SONGEA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA

Na Hasani Haufi – Mahakama, Songea.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha hivi karibuni amefanya ziara ya ukaguzi katika Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo mkoani Ruvuma.

Mhe. Karayemaha alifanya ukaguzi katika Mahakama za Wilaya Nyasa, Mbinga, Namtumbo na Tunduru pamoja na Mahakama za Mwanzo Namabengo, Luegu, Mkongo, Nakapanya, Nandembo, Matemanga, Ndegu na Mbambabay na kutembelea ofisi ya Mkuu wa Wilaya Tunduru.

Akiwa katika Mahakama hizo, Mhe. Karayemaha alipokea taarifa ya utekelezaji wa mashauri na utawala ambapo aliwapongeza watumishi wa Mahakama Kanda ya Songea kwa jitihada zao katika utendaji kazi.

Alisema kuwa jitihada hizo zimesaidia kiwango cha umalizaji wa mashauri kupanda kutoka asilimia  96.5% hadi kufikia asilimia 98.5% katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka

Sambamba na hayo, Jaji Mfawidhi alisisitiza watumishi kuwa weredi, wafanisi, waadilifu na wawajibikaji na wajitahidi kusoma, kuuelewa na kuuishi mpango mkakati wa Mahakama.

“Kufanya kazi kwa weredi, uadilifu na ufanisi sio ombi bali ni wajibu kwa kila mtumishi wa umma, ili kufikia malengo ya taasisi mnapaswa kutekeleza majukumu yenu kupitia misingi hiyo, pamoja na kusoma, kuuelewa na kuuishi mpango mkakati wa Mahakama ili kuendana na mabadiliko yaliyomo ndani ya mpango huo, lengo ni kupata matokeo chanya,” alisema.

Aidha, Mhe. Karayemaha alisisitiza ushirikiano kitaaluma katika utendaji kazi na kwa watumishi kujiunga kwenye vyama vya kitaaluma ili kuongeza weredi katika utendaji wao wa kazi.

“Kufikia malengo ya taasisi kunahitaji watumishi kutekeleza majukumu mnayopewa kwa ushirikiano, pia kwa lengo la kuongeza ufanisi na weredi mnapaswa kujiunga na kushiriki kwenye vyama vya taaluma kwani mtapata mambo na mbinu mpya tofauti tofauti ambazo zitakuongezea ujuzi,’’ alisema.

Viongozi wengine ambao aliambatana nao katika ziara hiyo Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea, Mhe. Elizabeth Nyembele, Mtendaji wa Mahakama, Bw. Epaphras Tenganamba, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Hakimu Mkazi Songea, Mhe. Japhet Manyama na Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi Kanda ya Songea, Mhe. Lilian Haule.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akikagua maeneo ya Mahakama ya Wilaya Mbinga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akipokea taarifa kutoka kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbinga (wa pili kutoka kushoto).

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Mbinga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akisalimiana na watumishi Mahakama ya Wilaya Nyasa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Mkongo iliyopo Wilaya ya Namtumbo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akitembezwa eneo la mMhakama ya Mwanzo Namabengo iliyopo Namtumbo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akipokea taarifa kutoka kwa Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbambabay (watatu kutoka kushoto).

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akisalimiana na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Tunduru.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru (wa kwanza kutoka kulia kwenye safu ya mbele).

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya Wilaya Namtumbo.

(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni