Na Naumi Shekilindi-Mahakama, Simiyu
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali hivi
karibuni alifanya ziara ya siku tano kukagua shughuli za kimahakama katika
Mahakama zote 42 zilizopo Mkoa wa Simiyu.
Katika
ziara hiyo, Mhe. Mahimbali aliongozana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Simiyu, Mhe. Martha Mahumbuga, Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Simiyu, Bw. Gasto Kanyairita pamoja na Katibu wake, Mhe. Dushi Lugoye.
Akizungumza
katika kikao cha majumuisho ya ziara yake, Jaji Mfawidhi alihimiza Mahakimu
kufunga mashauri ya mirathi yaliamuliwa baada ya miezi minne kukamilika.
Kadhalika,
Mhe. Mahimbali aliwaaziagiza Viongozi wa Mahakama katika ngazi zote kudhibiti
mipaka ya viwanja vya Mahakama na kurejesha maeneo yaliyonyang’anywa.
Alisisitiza
watumishi kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji na kuendeleza ushirikiano
baina yao, kutumia rasilimali kwa uangalifu na ubunifu ili kufikia adhma ya
Mahakama ya kutoa huduma bora kwa wananchi.
“Niwapongeze
wote kwa kujituma na kazi kubwa mnayoifanya, kwani licha ya kuwa na mazingira
magumu ya kazi na kwa uchache wenu bado mnafanya kazi ya kuhakikisha mnatoa
huduma bora,” aliwaambia watumishi wa Mahakama.
Akiwa
katika ziara hiyo, Jaji Mfawidhi alihimiza utekelezaji wa agizo la Jaji Mkuu la
kuongeza kasi ya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na
kuhakikisha kila Mahakama ya Mwanzo inawekewa huduma ya umeme.
Mhe.
Mahimbali pia alisisitiza matumizi ya watumishi wa kada moja kufanya kazi za
kada nyingine ili kujengea uwezo mwingine wa watumishi hao.
Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu aliwasilisha shukrani kwa niaba ya Mkoa wa Simiyu kwa ujio wa Jaji Mfawidhi na aliahidi kusimamia utekelezaji wa maagizo yote yaliyotolewa.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali akiwa
katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali alioongozana nao katika ziara
yake, akiwemo Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu Mhe. Martha
Mahumbuga (kushoto).
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali (katikati aliyeshika diari nyekundu) akikagua maeneo ya Mahakama Wilaya ya Maswa.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali akisikiliza
taarifa ya kituo cha Mahakama ya Mwanzo Itinje Wilaya ya Meatu.
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Maswa (aliyesimama) akimsomea taarifa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali (aliyekaa mbele) na pembeni ni Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, Mhe. Martha Mahumbuga.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Shinyanga, Mhe. Frank Mahimbali akithitimishi
ziara yake katika viwanja vya Maswa.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni