Na Evelina Odemba – Mahakama Morogoro
Majaji, Mahakimu,
waendesha mashtaka wa Serikali na
wapelelezi wameendelea kupigwa msasa wa masuala mazima ya upelelezi wa kesi.
Ni katika mafunzo yanayoendelea
kutolewa kupitia Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na
shirika lisilo la Kiserikali la pams foundation.
Akitoa somo leo tarehe 10
Oktoba, 2023 mwezeshaji Bw. Colman Lubisi Afisa Upelelezi toka Taasisi ya Kuzuia
na kupambana na rushwa TAKUKURU alisisitiza kuwa wanapotekeleza majukumu yao
wafanye kwa kuzingatia taaruma inavyowataka.
Bw. Lubisi aliendelea
kuelezea kuwa ni vyema shahidi akaandaliwa mapema ili kuhakikisha mshatakiwa
anapatiwa haki yake kwakuwa kesi nyingi hasa za ujangili huondolewa mahakamani
kutokana na kuwa ushahidi haujakamilika.
Akichangia mada wakati wa
kipindi cha majadiliano, Jaji wa Mahakama Kuu Mhe. Dkt. Deo Nangela alisema
kuwa ni muhimu kumuandaa shahidi mapema kabla ya kuingia naye mahakamani.
“Simaanishi umfundishe
shahidi akaseme nini isipokuwa kama mwendesha mashtaka unatakiwa kujua shahidi
anaenda kusema nini mahakamani na endepo ana kumbukumbu ya anachoenda kutolea ushahidi,”
alifafanua Mhe. Nangela.
Kuhusu suala la usalama
kwa mashahidi, Mhe. Nangela alishauri wapelelezi kutumia utambulisho wa
mashahidi zaidi tofauti na kumleta shahidi mbele ya Mahakama kwa kuwa
utambulisho huo utakuwa unafahamika kimahakama, hii ni katika mashauri ambayo
shahidi anahofia usalama wa maisha yake.
Ikumbukwe kuwa mafunzo
haya yamejikita katika mashauri ya makosa ya wanayamapori na maliasili ambayo
yatatolewa hapa na yanatarajiwa kuhitimishwa mnamo tarehe 13 Oktoba,2023.
Lengo likiwa ni kuwajengea ujuzi na kubadilishana uzoefu kwakuwa washiriki toka maeneo mbalimbali wakiwemo Majaji wa Mahakama Kuu, Mahakimu, Waendesha Mashataka na wapelelezi wamekutana pamoja.
Muwezeshaji wa mafunzo,
Bw. Colman Lubisi, Afisa Mwandamizi wa Upelelezi toka Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) akitoa somo kwa washiriki wa mafunzo (hawapo
pichani).
Mwezeshaji (juu na chini) akiendelea
kutoa mafunzo kwa washiriki.
Jaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Mhe. Dkt Deo Nangela akichangia mada wakati wa mafunzo.
Washiriki wa mafunzo
wakifuatilia mada toka kwa muwezeshaji (hayupo pichani).
Darasa likiendelea.
Jaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania (kushoto) Mhe. Rose Ebrahim ambaye ni miongoni mwa washiriki wa
mafunzo akifuatilia kwa makini.
Jaji wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Mhe. Mwanabaraka Mnyukwa (wa kwanza kulia) pamoja na washiri
wakifuatilia mafunzo.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni