Na Arapha Rusheke, Mahakama Kuu, Dodoma
Mahakama Mkoa wa Dodoma jana
tarehe 9 Octoba, 2023 iliendesha mafunzo kwa vitendo kwa watumishi ili
kuwajengea uelewa wa matumizi sahihi ya mfumo mpya ulioboresha (E-Advanced Case
Management) wa kupokea na kuratibu mashauri yote yanayopokelewa mahakamani.
Mafunzo hayo yalifunguliwa na Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Adam Mambi katika ukumbi wa mikutano kwenye Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma.
Akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo, Mhe. Dkt. Mambi aliwataka washiriki kusikiliza kwa makini ili waweze kuuelewa mfumo huo mpya ambao umeboreshwa kufuatilia mwenendo wa shauri tangu linapofunguliwa hadi kumalizika kwake.
“Huu ni mfumo mpya, tuna hama kutoka katika mfumo wa mwanzo wa JSDS II na sasa tunaenda kwenye mfumo wa kisasa wa E-case Management. Hii itarahisisha wananchi kupata kitu chochote cha Mahakama kwa urahisi kabisa,” alisema.
Kaimu Jaji Mfawidhi alibainisha kuwa kuanzishwa kwa mfumo huo mpya ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Jaji Mkuu na mpango mkakati wa Mahakama.
Mafunzo hayo yalihudhuriwa na watumishi katika Mkoa wa Dodoma, wakiwemo kutoka Mahakama Kuu Dodoma, Mahakama za Wilaya Bahi, Kongwa,Chemba, Mpwapwa na Kondoa.
Kwa upande wa Mahakama Kuu, waliohudhuria ni Majaji, Naibu Msajili, Mtendaji, Afisa Utumishi na wengine huku kutoka katika kila Wilaya alikuwepo Hakimu Mfawidhi, Afisa Utumishi pamoja na Karani.
Alikuwepo pia Afisa Tehama, Bi. Amina Said kutoka Kituo Jumuishi cha
Masuala ya Familia Temeke, ambaye ndiey alikuwa mtoa mada mkuu katika mafunzo
hayo.
Mtendaji wa Mahakamu Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Dodoma, Bw.Sumera Manoti (aliyesimama) akzungumza wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya washiriki waliohudhuria mafunzo hayo wakifuatilia mafunzo hayo.
Mkufunzi, Bi. Amina Said akieleza
jambo wakati wa mafunzo kwa watumishi wa Mahakama Mkoa wa Dodoma.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu
ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Adam Mambi (aliesimama katikati) akiwa
katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo.
Mtendaji wa Mahakamu Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Dodoma, Bw. Sumera Manoti akifuatilia kwa umakaini mafunzo ya E-Case management.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe Sylvia Lushasi (wa kwanza kushoto) akiwa na
Mtunza Kumbukumbu Mwandamiz,i Bi. Fatmah Nkamirwa wakati wa mafunzo hayo.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni