·Yashika nafasi ya nne
·Mpira wa miguu waachia ndugu zao Sheria mshindi wa tatu
Na
Faustine Kapama-Mahakama, Iringa
Timu ya Mahakama ya Tanzania
(Mahakama Sports) Netiboli imeweka historia mpya kwenye Mashindano ya
Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayofanyika
mkoani hapa baada ya kushika nafasi ya nne katika mchezo huo.
Mahakama Sports imefika
katika hatua hiyo baada ya kutolewa na Hazina, ambayo imeshika nafasi ya tatu
kufuatia mchezo mgumu uliochezwa kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Kikatoliki Ruaha
leo tarehe 12 Octoba, 2023 kuanzia saa 10:00 jioni.
Pamoja na kucheza pungufu
mchezaji mmoja katika kipindi cha pili, Mahakama Sports iliweza kumudu vyema
mchezo huo ambao ulikuwa piga nikupige kwani timu moja inapotumbukiza kikapu, timu
nyingine nayo inajibu mapigo.
Mchezaji mmoja wa
Mahakama Sports alitolewa nje kufuatia figisufigisu za waamuzi, hivyo kuwafanya
wachezaji wa Hazina wawe wengi zaidi uwanjani na kuwawezesha kuutawala mchezo.
Hadi mchezo unamalizika, Hazina
walifanikiwa kutumbukiza vikapu 39, huku Mahakama Sports ikawa imevuna vikapu
30, jambo lililotafasiliwa na watazamaji kuwa matokeo yasingekuwa hivyo kama
timu zote zingekuwa na wachezaji sawa.
Kitendo cha Mahakama
Sports kushika nafasi hiyo kinaifanya kuweka historia mpya SHIMIWI kwani mwaka
jana kwenye mashindano hayo yaliyofanyika jijini Tanga iliishia katika hatua ya
16 bora.
Katika hatua nyingine, Mahakama
Sports mpira wa miguu imewaachia ndugu zao Sheria kushika nafasi ya tatu kwenye
mashindano hayo baada ya kumalizika kwa mchezo kabambe uliozikutanisha timu
hizo.
Mchezo huo iliochezwa katika
uwanja wa Samora kuanzia saa 10:00 jioni ulikuwa wa kuvutia kwani timu hizo
ndugu zilicheza kiistarabu na hapakuwepo na purukushani za hapa na pale kwa
wachezaji.
Ilikuwa Mahakama Sports
iliyokuwa ya kwanza kuliona lango la ndugu zao kabla nao kujipu mapigo na
kusawazisha kutokana na mpira wa adhabu ulioelekezwa langoni na kumpita mlinga
mlango alipokuwa anajaribu kuokoa hatari hiyo.
Hadi kipindi cha kwanza
kinamalizika, timu zote zilienda kwenye mapumziko zikiwa na nguvu sawa. Katika
kipindi cha pili, Mahakama Sports waliweza kumiliki mpira na kushambulia lango
la wapinzani mara kwa mara.
Hata hivyo, bahati ya
kupachika mabao haikuwa yao, jambo lililowapa faida Sheria na kutumia moja ya
nafasi chache walizozipata kupata bao la pili na la kuongoza kutokana na adhabu
ndogo iliyoelekezwa kwenye lango lao.
Hadi mwamuzi anapuliza
kipenga kuashiria kumalizika kwa mtanange huo, Sheria wakaibuka washindi wa bao
2:1.
Kufuatia matokeao hayo,
Mahakama Sports inashika nafasi ya nne kwenye mchezo huo na Sheria inakamata
nafasi ya tatu. Fainali za mpambano huo zinatarajiwa kufanyika kesho tarehe 13
Octoba, 2023 kuzikutanisha Hazina na Mifugo.
Mkata umeme akageuka nyuma akamkuta mshambuliaji wa kati Nyangi Kisangeta.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni