Ijumaa, 13 Oktoba 2023

MSAIDIZI MKUU OFISI MAHAKAMA YA MWANZO MINGOYO LINDI AFARIKI DUNIA

 

                                                               TANZIA

Bw. SALUMU MZEE AMLANI Enzi za Uhai wake.

Uongozi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi kwa masikitiko makubwa unatangaza kifo cha mtumishi Bw.SALUMU MZEE AMLAN- Msaidizi Mkuu wa Ofisi mwenye Check No.8956996 kutoka Mahakama ya Mwanzo Mingoyo iliyopo wilaya ya Lindi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Uongozi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi imeeleza maheremu SALUMU MZEE AMLANI amefariki dunia tarehe 12 Oktoba, 2023 katika Hospitali ya Ndanda alipokuwa akipatiwa matibabu.

Mazishi yake yatafanyika leo tarehe 13 Oktoba, 2023 majira ya saa 10 jioni Mtwara Mjini.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni