Alhamisi, 12 Oktoba 2023

MAHAKAMA YA MWANZO KILEMA KUFANYIWA UKARABATI MKUBWA

Na. Paul Pascal –Mahakama, Moshi

Uongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi kwa kushirikisha na wananchi wa Kata ya Kilema Wilaya ya Moshi vijijini mkoani Kilimanjaro umeratibu zoezi la ukarabati mkubwa wa jengo chakavu la Mahakama ya Mwanzo lililopo Kata hiyo ili kuwezesha wananchi kupata huduma za kimahakama zilizositishwa toka mwaka 2018 kutokana na uchavu wa jengo hilo.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika hivi karibuni cha kuanzisha mchakato wa utekelezaji wa ukarabati mkubwa wa jengo hilo, Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi Bw. Donald Makawia alitoa rai kwa viongozi na wananchi wa Kata ya Kilema kushirikiana bega kwa bega na kuunganisha nguvu kwa pamoja ili kurejesha jengo hilo katika muonekano nadhifu na salama kwa ajili ya kuhakikisha wananchi wanapata jengo bora la kutolea huduma ya haki.

“Itakubukwa Mahakama hii ya kilema ilifungwa mwaka 2018 kutokana na uchakavu mkubwa hivyo kushindwa kutumika kutolea huduma za kimahakama. Lakini mnamo mwaka 2023 Mahakama hii iliweza kufunguliwa na kufanya shughuli zake kupitia jengo la kuazimwa linalomilikiwa na Serikali ya Kijiji kutokana na uhitaji wa huduma za kimahakama”, alisema Mtendaji huyo.

Mtendaji Makawia alisema, ukarabati huo utajumuisha uvunjaji wa jengo la zamani, ujenzi wa ukumbi wa wazi, ukarabati wa vyumba viwili vya waheshimiwa Mahakimu, ukarabati wa chumba cha masijala, ukarabati wa chumba cha mahabusu pamoja na uwekaji wa miundombinu ya maji na umeme.

Ukarabati na ujenzi huo umetengewa kiasi cha fedha shilingi milioni 17 ambazo zimetolewa toka Ofisi ya Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania (MMK - K) baada ya kutembelea na kukagua Mahakama hiyo kwa maombi ya mtendaji wa mahakama kuu kanda ya moshi mwezi augusti 2023. Aliongeza Bw. Makawia

Aidha, Sambamba na mchango huo kutoka Ofisi ya Mtendaji wa Mahakama Kuu. Mahakama Kuu Kanda ya Moshi imeungana na uongozi wa kata ya Kilema ikiwa ni utekelezaji wa nguzo ya pili ya Mpango Mkakati wa Mahakama upatikanaji  wa huduma za utoaji haki kwa wakati, maeneo ya matokeo muhimu (ushirikishwaji wa wadau, majengo na miundo mbinu).

Ukarabati huo ulioanza kutekelezwa mnamo tarehe 10 Oktoba, 2023 na utafanywa kwa kutumia nguvu kazi ya wananchi na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2023.

Muonekano wa sasa wa jengo la Mahakama ya Mwanzo kilema iliyofungwa mwaka 2018 kutokana na uchakavu mkubwa na kushindwa kutumika kutolea huduma za kimahakama.

Mafundi wakiendelea na shughuli za ukarabati Mahakama hiyo iliyofungwa mwaka 2018 kutokana na uchakavu huo.

Mafundi wakiendelea na shughuli za ukarabati Mahakama hiyo iliyofungwa mwaka 2018 kutokana na uchakavu huo.

Mafundi wakiendelea na shughuli za ukarabati Mahakama hiyo iliyofungwa mwaka 2018 kutokana na uchakavu huo.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni