Na Evelina Odemba – Mahakama Morogoro
Menejimenti Kuu ya
Mahakama ya Tanzania imekutana mkoani hapa leo tarehe 7 Oktoba, 2023, kujadili
masuala mbalimbali ya msingi ya kiutendaji.
Katika kikao hicho, Mwenyekiti
wake ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole
Gabriel alisisitiza kuendelea kuboresha huduma za upatikanaji wa haki kwa
wananchi.
Menejimenti hiyo inaundwa
na wakuu wa idara na vitengo vyote ndani ya Mahakama ya Tanzania, huku
Mwenyekiti Mwenza akiwa ni Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Sylvester Kainda.
Kwa upande wake, Mhe.
Kainda alizungumzia suala la mashauri na kueleza kuwa Mahakama ya Rufani imeboresha
utoaji wa takwimu tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Kikao hicho pia kilipokea
taarifa mbalimbali za uwajibikaji ambazo zimefanyiwa kazi kama ilivyoazimiwa na
kikao kilichopita. Taarifa hiyo ilisomwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali
Watu wa Mahakama ya Tanzania, Bi. Beatrice Patrick.
Mahakama ya Tanzania, kupitia mpango mkakati wake, imejikita katika uboreshaji wa huduma mbalimbali, ikiwemo majengo. Miongoni mwa maboresho hayo ni uwepo wa Vituo Jumuishi vya Utoaji Haki (IJCs).
Viongozi wa Menejimenti Kuu
ya Mahakama ya Tanzania, akiwemo Mwenyekiti wa Kikao ambaye ni Mtendaji Makuu
wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabrie (katikati), Mwenyekiti
Mwenza, ambaye ni Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Sylvester Kainda (kulia) na
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Mahakama ya Tanzania, Bi. Beatrice
Patrick, wakifuatilia yaliyokuwa yanajiri kwenye kikao.
Wajumbe wa kikao cha
Menejimenti Kuu ya Mahakama wakipiga makofi wakati Katibu wa Kikao, Bi.
Beatrice Patrick (aliyesimama mbele) akiwapitisha katika taarifa fupi ya
masuala yaliyotekelezwa na Mahakama ya Tanzania pamoja na mrejesho wa taarifa
ya kikao kilichopita.
Mjumbe wa kikao cha
Menejimenti Kuu ya Mahakama ya Tanzania akichangia hoja.
Mwenyekiti Mwenza wa Kikao
cha Menejimenti Kuu ya Mahakama ya Tanzania, ambaye pia ni Msajili wa Mahakama
ya Rufani, Mhe. Sylivester Kainda akifuatilia kinachoendelea kwenye kikao.
Katibu wa Kikao cha Menejimenti
Kuu ya Mahakama ya Tanzania, Bi. Beatrice Patrick akichangia mada wakati wa
kikao.
Sekretarieti ya Kikao cha
Menejimenti Kuu ya Mahakama ya Tanzania wakati wa kikao.
Sehemu ya wajumbe wa Menejimenti
Kuu ya Mahakama ya Tanzania ikiwa katika kikao.
Mjumbe wa Menejimenti Kuu
ya Mahakama ya Tanzania akichangia mada.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Iringa)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni