Na Lydia Churi- Tume ya Utumishi wa Mahakama- Kagera
Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati
ya Maadili ya Maafisa Mahakama ngazi ya Mkoa Mhe. Fatma Mwassa amesema mkoa wa
Kagera unaridhishwa na utendaji kazi wa Mahakama ya Tanzania.
Akizungumza na Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume
ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma mara baada ya kumpokea
katika kiwanja cha Ndege cha mjini Bukoba, Mkuu huyo wa Mkoa alisema wana
Kagera wanaridhishwa na Utendaji kazi wa Mahakama na kasi ya kushughulikia
migogoro na mashauri ni kubwa.
”Sisi wana Kagera pamoja na kuwa tuna kesi nyingi zile
ngumu lakina tunaridhishwa sana na utendaji kazi wa Mahakama ya Tanzania”,
alisema Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Alisema mkoa wa Kagera umeanza jitihada za kupunguza
migogoro ile ambayo si lazima ifike mahakamani. Aliongeza kuwa wamejipanga kutoa
mafunzo maalum kwa Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na viongozi
wengine ili kuwajengea uwezo wa namna ya kushughulikia migogoro midogo midogo
ambayo haina ulazima wa kufikishwa mahakamani. Mafunzo hayo yatatolewa na Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba.
Akielezea hali ya mauaji katika mkoa wa Kagera, Mhe.
Mwassa alisema hivi sasa mkoa wake unaendesha kampeni kubwa ya kudhibiti mauaji
na kwamba vitendo hivyo vimepungua na kwa mujibu wa ripoti ya Polisi, mkoa huo
umetoka kuwa mkoa unaoongoza kwa kuwa na kesi nyingi za mauaji.
Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania alisema Makamishna
wa Tume wamewasili mkoani Kagera kuanza ziara katika mikoa ya Kagera na Geita yenye
lengo la kukutana na Wajumbe wa Kamati
za Maadili ya Maafisa Mahakama ili kuimarisha utendaji kazi wa kamati hizo
ikiwa ni panoja na kuangalia maeneo yanayohitaji mabadiliko ya kanuni.
”Tume iko Dar es salaam lakini shughuli nyingi za
usimamizi wa maadili ya Maafisa Mahakama zinafanyika nchini kote, viongozi wa
mikoa na wilaya ni wawakilishi wa Tume”, alisema Jaji Mkuu.
Alisema katika ziara ya Tume kwenye mikoa ya Kagera na
Geita, Makamishna wa Tume pia watapata nafasi ya kukutana na Watumishi wa
Mahakama pamoja na viongozi na kuangalia maeneo yanayohitaji miundiombinu ya
Mahakama ili kuboresha huduma za utoaji haki.
Tume ya Utumishi wa Mahakama inatarajiwa kuanzia ziara ya
siku nne katika mikoa ya Kagera na Geita yenye lengo la kuimarisha utendaji
kazi wa Kamati za Maadili ya Maafisa Mahakama. Ziara hiyo itaanza kesho tarehe 9
Oktoba na kumalizika tarehe 12 Oktoba, 2023.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati
ya Maadili ya Maafisa Mahakama Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa akimpokea Jaji
Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Prof.
Ibrahim Hamis Juma alipowasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo Tarehe 8 Oktoba, 2023 kuanza ziara ya siku nne ya Tume katika
mikoa ya Kagera na Geita yenye lengo la kuziimarisha Kamati za Maadili ya
Maafisa Mahakama.
Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo Tarehe 8 Oktoba, 2023 kuanza ziara ya siku nne ya Tume ya Utumishi wa Mahakama katika mikoa ya Kagera na Geita yenye lengo la kuziimarisha Kamati za Maadili ya Maafisa Mahakama. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Maafisa Mahakama Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa akizungumza na Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Mhe. Prof.
Ibrahim Hamis Juma pamoja na Makamishna wengine wa Tume (hawapo pichani) mara baada ya kuwapokea katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo Tarehe 8 Oktoba, 2023.
Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi
wa Mahakama Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwasili katika uwanja wa ndege wa
Bukoba leo Tarehe 8 Oktoba, 2023 kuanza ziara ya siku nne ya Tume ya
Utumishi wa Mahakama katika mikoa ya Kagera na Geita yenye lengo la
kuziimarisha Kamati za Maadili ya Maafisa Mahakama.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu ya Tanzania Mhe. Immaculate
Banzi akimpokea Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa
Mahakama Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alipowasili katika uwanja wa ndege wa
Bukoba kuanza ziara ya siku nne ya Tume ya Utumishi wa Mahakama katika mikoa ya
Kagera na Geita. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Bw. Toba Nguvila.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania na Katibu wa Tume
ya Utumishi wa Mahakama Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) mara baada ya
kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba kuanza ziara ya siku nne ya Tume ya
Utumishi wa Mahakama katika mikoa ya Kagera na Geita. Kushoto ni Jaji Mfawidhi
wa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba Mhe. Immaculate Banzi na katikati ni Katibu Tawala
wa Mkoa wa Kagera Bw. Toba Nguvila.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni