Na Naumi Shekilindi-Mahakama, Simiyu
Mtendaji
wa Mahakama Mkoa wa Simiyu, Bw. Gasto Kanyairita jana tarehe 17 Octoba, 2023 ametembelea
na kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la Mahakama ya Wilaya Maswa mkoani hapa
na kuhimiza kazi hiyo kukamilika haraka.
Katika
ziara hiyo ya ukaguzi, Bw. Kanyairita aliambatana na Hakimu Mfawidhi wa
Mahakama ya Wilaya Maswa, Mhe Enos Missana, Mkaguzi wa Ndani, Bw. Kisasila
Nsukuma na Mkandarasi wa jengo hilo, Bw. Emmanuel Kileo kutoka Kampuni ya Great
Wall Construction Ltd.
Akizungumza
katika kikao baada ya kutembelea jengo hilo, Mtendaji alimsisitiza mkandarasi
kuzingatia tarehe aliyoahidi kukamilisha ujenzi ili jengo lianze kutumika
haraka iwezekanavyo.
Kwa
sasa Mahakama ya Wilaya Maswa inafanya kazi katika jengo la kukodi la shirika
la posta lililopo wilayani hapo.
“Jengo
hili litakapokamilika litaondoa gharama zinazotumika kulipa kodi katika jengo la
kukodi, hivyo pesa hizo zitaweza kutumika kuendelea kukarabati na kutengeneza
miundombinu katika Mahakama za Mwanzo zilizopo wilayani hapa,” alisema Bw.
Kanyairita.
Sambamba
na ukaguzi huo, Bw. Kanyairita alipita kuwasalimu watumishi wa Mahakama ya Wilaya
Maswa na kuwasihi waendelee kufanya kazi kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji
ili kufikia dira ya Mahakama ya utoaji haki kwa wakati.
Ukarabati
wa jengo hilo ulianza tarehe 1 Agosti, 2022 na kutakiwa kuisha tarehe 30
Novemba, 2022, lakini kutokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa nje ya
uwezo, jengo hilo linatarajiwa kukamilika Oktoba, 2023.
Ukarabati
wa jengo hilo unafanyika kutokana na fedha za za ndani, hii ni fahari kubwa
kuona Mahakama inafanya juhudi ya kuwawezesha watumishi wafanye kazi katika
mazingira mazuri na kutoa huduma bora kwa wateja.
Kazi
ya ukarabati kwa sasa umefikia asilimia 89 na mkandarasi ameahidi kukamilisha
ujenzi huo katika kipindi kifupi kijacho.
Mahakama
ya Tanzania inatekeleza mkakati wake wa kuboresha miundombinu, ikiwemo ujenzi
wa majengo ya kisasa ili kuimarisha huduma za utoaji haki kwa wananchi.
Muonekano
wa jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Maswa kwa upande.
Mtendaji
wa Mahakama Mkoa wa Simiyu, Bw.
Gasto Kanyairita (wa pili kushoto) akizungumza na wakandarasi pamoja na Mkaguzi wa Ndani wakati
wa ukaguzi wa jengo hilo.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni