Na James Kapele-Mahakama, Katavi
Watumishi wa Mahakama
Mkoa wa Katavi leo tarehe 13 Octoba, 2023 wamepata elimu ya masuala ya afya ya macho,
pua, masikio, na mfumo wa koo kutoka kwa madaktari bingwa wa Hospitali ya Rufaa
ya Katavi.
Shughuli hiyo imefanyika
katika ukumbi wa wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi kwa lengo la kutoa
elimu kuhusu visababishi vya magonjwa yanayoathiri sehemu hizo muhimu za mwili
wa binadamu na nanmna ya kujikinga na kisha kufanya vipimo bure kwa watumishi
walioshiriki katika mafunzo hayo.
Madaktari bingwa
waliongoza mafunzo hayo ni Dkt. Salome Renatus ambaye ni Mratibu wa Huduma ya Macho
wa Hospitali ya Rufaa ya Katavi na Dkt. Noela Lema wa Kitengo cha Pua na Masikio
katika hospitali hiyo.
Akizungumza wakati anatoa
elimu ya macho, Dkt. Salome amesisitiza kwamba watumiaji wengi, hasa wa
kompyuta wamekuwa wahanga wakubwa wa magonjwa ya macho kwa kuwa wengi hawajapa
elimu ya nanma sahihi ya matumizi ya vifaa hivyo.
“Wengi wenu hapa mnatumia
kompyuta na kila mtu anaitumia kulingana na namna macho yake yanavyotaka au
meza na kiti anachotumia. Lakini nawashauri wekeni kompyuta zenu umbali wa urefu
wa mkono wako ili mwanga usilete madhara ya moja kwa moja kwenye macho yenu,”
alisema.
Mafunzo hayo
yalifunguliwa na Afisa Utumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi, Bw. Ayubu
Nyalobi ambaye alibainisha kuwa ofisi inatambua umuhimu wa watumishi kuwa na
afya njema na ndiyo lengo la kuomba wataalamu hao wafike kufanya kazi hiyo.
Ameeleza kwamba ofisi
itaendelea kuleta wataalam mbalimbali wa afya ili elimu kuhusu maeneo
mbalimbali ya kiafya iwafikie watumishi, kwani ubora wa afya zao utaongeza
ufanisi wa kazi na majukumu yao ya kila siku.
Pichani ni aliyeketi ni moja kati ya watumishi wa Mahakaka, Bw. Josiah Mwalongo akipata vipimo katika baada ya mafunzo hayo.
(Habari
hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni