Na Hasani Haufi- Mahakama, Songea
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe. James Karayemaha jana tarehe 1 Novemba,
2023 amewahimiza watumishi wote wa Mahakama katika Kanda hiyo kushiriki katika
mazoezi kwani ndiyo mwarobaini wa kuimarisha afya.
Mhe. Karayemaha ametoa
wito huo jana tarehe 1 Novemba, 2023 wakati akizungumza na baadhi ya watumishi
wa Mahakama Kuu katika hafla ya uzinduzi wa mazoezi kwa watumishi wa Mahakama
Kanda ya Songea.
“Afya bora na imara
hujengwa na kuboreshwa kwa mambo mbalimbali, lakini mazoezi kwa binadamu
yamekuwa ni tiba na mwarobaini wa kuboresha na kujenga afya ya mwanadamu,’’ alimesema.
Jaji Mfawidhi alisema
kuwa afya ni mtaji na utajiri mkubwa kwa binadamu, hivyo watumishi wote wanapaswa
kulinda tunu waliyopewa na Mungu na njia pekee ya kufanikisha jambo hilo ni
kufanya mazoezi ya mara kwa mara.
“Muda mwingi tunautumia
kukaa sehemu moja, hivyo ni rahisi kupata tatizo la afya na ili kuepukana na
changamoto hiyo tunapaswa kufanya mazoezi kila siku,” alisema.
Aliwakumbusha pia matumizi
ya vyakula, ikiwemo vya wanga wanavyotumia kila siku ambavyo baada ya mfumo wa
umeng’enywaji hutengeneza sukari na mafuta, hivyo ili kulinda afya kutokana na
tatizo la magonjwa kama sukari na shinikizo la damu (pressure) wanapaswa
kufanya mazoezi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni