Christopher Msagati – Mahakama, Manyara
Wananchi
mjini Babati mkoani Manyara wameipongeza Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya
Manyara kwa kuboresha huduma zinazotolewa kila siku Mahakamani.
Pongezi
hizo zimetolewa leo tarehe 2 Novemba, 2023 wakati Wananchi wakipokea Elimu
inayotolewa kila siku ya Alhamisi kabla ya kuanza kwa shughuli za usikilizaji
wa mashauri katika viwanja vya Mahakama Kuu Manyara.
“Kwa
kweli siku hizi Mahakama imebadilika kwa namna ambavyo mnatoa huduma zenu
tofauti na zamani, hata huu mfumo wa kutuelimisha kila tunapofika Mahakamani
unaonesha kuwa kweli mna nia ya kurejesha imani kwa Wananchi kwa sababu pia
mnatufundisha taratibu mbalimbali ambazo tulikuwa hatuzifahamu hapo awali kwa
hili mnastahili pongezi”, amesema Bw. Beatha Temu ambaye ni mmoja wapo wa
wananchi waliohudhuria Mahakamani.
Akitoa
mada kwa wananchi hao Msaidi wa Sheria Mahakama Kuu Manyara, Mhe. Thobias John aliwafundisha
wananchi juu ya ‘TARATIBU ZA UKATAJI WA RUFAA KATIKA MAHAKAMA’ huku
akiwasisitiza kuwa taratibu hizi huwa zinatofautiana kulingana na ngazi ya
Mahakama husika.
“Ni
vema kuzingatia haya ninayowafundisha sasa hivi kwa sababu ukifika Mahakama ya
Wilaya utakuta taratibu zake za kukata rufaa zinatofautiana kidogo na zile za
Mahakama Kuu”, amesema Mhe. John.
Mahakama
Kuu Kanda ya Manyara imejiwekea utaratibu wa kutoa elimu kwa Wananchi wanaofika
Mahakamani kila ya siku ya Alhamisi kuanzia saa 2 asubuhi kabla ya shughuli ya
usikilizaji wa Mashauri haijaanza.
Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mhe.
Thobias John akitoa Elimu kwa Wananchi waliohudhuria Mahakamani (hawapo picha) ikiwa ni utaratibu wa Mahakama Kuu Kanda ya Manya kila siku ya Alhamisi saa 2 asubuhi.
Sehemu
ya Wananchi waliofika Mahakama Kuu Manyara wakisikiliza elimu iliyokuwa
ikitolewa kabla ya kuanza kusikilizaji wa mashauri.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni