Jumatano, 6 Desemba 2023

MBEYA YASHIRIKI KAMPENI YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA MITANDAONI

Mwinga Mpoli – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dustan Ndunguru amewakumbusha wadau juu ya makosa yanayotendeka kimtandao na kuwa nchi ilitunga sheria mahususi juu ya makosa hayo, hivyo ni wajibu wetu kama wadau wa haki kusimama na kukemea vitendo hivi ukatili wa kijinsia.

Ameyasema hayo hivi karibuni akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto, ambapo chama cha Majaji na Mahakimu wanawake Tanzania (TAWJA), kiliandaa zoezi la Mahakama ya Mfano na kuendesha kesi ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ambapo kauli mbiu ilikuwa ni “kupinga unyanyasaji na ukatili wa kijinsia mitandaoni”. Zoezi ili lilihusisha waheshimiwa majaji, mahakimu, mawakili wa serikali, mawakili wa kujitegemea, polisi, wakufunzi na wanafunzi wa vyuo vikuu Mzumbe na CUCoM mkoa wa Mbeya.

 “Nimefurahi kuona kuwa mmeshirikisha watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi na naamini zoezi ili la Mahakama ya mfano litasaidia kujua makosa ya kimitandao, mara nyingi tunajisahau na kuhisi tunafanya utani ila ni muhimu tukumbuke kuna madhara ya maneno yetu mitandaoni na ili suala limekuwa likituathiri na kama walengwa kwa pamoja tusimame kupinga unyanyasi na ukatili wa kijinsia. Tuelimike lakini pia tuielimishe jamii inayotuzunguka” alisema Mhe. Ndunguru

Pia alishukuru TAWJA, Mahakama ya Tanzania na washiriki wengine wote kwa kuona umuhimu wa kushiriki katika maadhimisho hayo ya kupinga unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Aidha uongozi wa TAWJA Mbeya ulisimamia na kuendesha zoezi ilo la Mahakama ya mfano ikiwa washiriki katika Mahakama hiyo wakiwa ni Mahakimu, mawakili wa serikali, Mawakili wa kujitegemea, mapolisi pamoja na wanafunzi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dustan Ndunguru akitoa hotuba ya ufunguzi wa zoezi la Mahakama ya Mfano kupinga unynyasaji wa kijinsia mitandaoni

Sehemu ya washiriki wa Mahakama ya Mfano wakiendesha shauri la unyanyasaji wa kijinsia mtandaoni.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Dustan Ndunguru (wapili kushoto) akiwa sehemu ya washiriki wa zoezi hilo la uendeshaji kesi ya Mahakama ya Mfano na watatu kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa akifuatilia na washiriki wengine.

sehemu ya washiriki wa zoezi hilo la uendeshaji kesi ya Mahakama ya Mfano wakifurahia jambo.

sehemu ya washiriki wa zoezi hilo la uendeshaji kesi ya Mahakama ya Mfano wakifuatilia zoezi hilo.


sehemu ya washiriki wa zoezi hilo la uendeshaji kesi ya Mahakama ya Mfano wakifuatilia kwa makini.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Mhe. Dustan Ndunguru (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau walioshiriki zoezi la uendeshaji wa Mahakama ya Mfano na wa kwanza kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha  Mahakama)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni