Jumamosi, 2 Desemba 2023

MTENDAJI MOSHI AKAGUA UKARABATI WA JENGO LA MAHAKAMA MWANZO KILEMA

Na. Paul Pascal – Mahakama, Moshi

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala amefanya ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.

Ukaguzi huo umefanyika tarehe 30 novemba 2023 ukiwa na lengo la kujionea maendeleo ya uboreshaji wa miundo mbinu ya Mahakama hiyo ili kuweka mazingira rafiki ya utoaji huduma kwa watumishi wa Mahakama pamoja na wananchi wa kata ya kilema kusini na vitongoji vya jirani vilivyopo katika Wilaya ya Moshi Vijijini.

“Nipende kuwahaikishia wananchi wote wa kilema kati na vijiji vya jirani ya kuwa mahkama ya Tanzania itahakikisha jengo hili linakua bora na zuri kwa matumizi yetu sote ili kuwezesha wananchi wote wanapata sehemu nzuri ya kupatia haki zao”, alisema Mtendaji huyo

Ukarabati wa Mahakama ya Mwanzo Kilema ulianza mwezi Oktoba 2023 na unatazamiwa kukamilika tarehe 15 Desemba 2023 ukitekelezwa kwa fedha za ndani kutoka ofisi ya Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi ukiwa na thamani ya milioni 17, kukamilika kwa ukarabati huu kutawezesha shughuli za kimahakama kufanyika katika jengo linalomilikiwa na Mahakama ya Tanzania. Kwa sasa shughuli za Mahakama ya Mwanzo Kilema zinaendeshwa katika jengo la serikali ya Kata ya Kilema Kusini.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala akifanya ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala akifanya ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala akifanya ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala akifanya ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya moshi Bi. Maria Itala akisaini kitabu cha wageni mara alipofika Mahakama ya Mwanzo kilema kabla ya kuanza zoezi la ukaguzi katika jengo linaloendelea kufanyiwa kukarabati la Mahakama ya Mwanzo Kilema.

Habari Hii imehaririwa na Innocent Kansha -Mahakama.


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni