Jumatatu, 29 Januari 2024

ELIMU WIKI YA SHERIA YAWAKOSHA WANANCHI MKOANI LINDI

Na. Hilary Lorry – Mahakama, Lindi

  •    Wafurahishwa na jitihada za Mahakama kuwafikia walipo.
  •    Wavutiwa na mada mbalimbali zinazowasilishwa na watoa elimu waliobobea     katika  masuala mbalimbali ya kisheria.
  •  Waipongeza mahakama kwa uwazi na huduma bora wanazozitoa.
  •   Waipongeza Mahakama kwa ushirikiano mzuri na wadau.

Viongozi wa Mahakama Mkoa wa Lindi wakiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano kwa nyakati tofauti walitoa wito kwa wananchi Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kwenye maadhimisho ya wiki ya sheria nchini ili kupata elimu na kujifunza mambo mbalimbali yanayofanywa na Mahakama katika mchakato mzima wa upatikanaji wa haki.

Wiki ya elimu inachagizwa na kauli mbiu isemayo “Umuhimu Wa Dhana Ya Haki Kwa Ustawi Wa Taifa: Nafasi Ya Mahakama Na Wadau Katika Kuboresha Mfumo Jumuishi Wa Haki Jinai’’

Katika kuitikia wito Wananchi mkoani Lindi wameendelea kujitokeza kwa wingi katika mabanda   ya maonyesho ya wiki ya sheria  yaliyopo mkabala na hotel ya sea view  katika viwanja vya mpira wa kikapu kupata msaada wa kisheria, elimu, kujua taratibu za kimahakama na mambo mengine kemkem yanayowasilishwa na watumishi wa Mahakama pamoja na wadau mbalimbali wanaoshiriki zoezi la utoaji elimu.

Aidha, wananchi wamefurahishwa na jitihada za Mahakama kuwafikia wananchi popote walipo kwa kutembelea maeneo ya mikusanyiko, mashuleni, vyuo, na kuwatenegenezea mazingira mazuri ya kupata elimu na vipindi mbalimbali vya redio. Vilevile walitoa pongezi za dhati kwa uwasilishwaji wa mada zinazogusa kila nyanja katika jamii zilizowasilishwa kwa kina na wabobezi katika tasnia ya sheria.

Sambamba na hilo, wananchi mkoani Lindi wameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa uwazi na huduma bora wanayoendelea kuitoa kwa wananchi. Na pia wamefurahishwa na ushirikishwaji mzuri wa wadau katika zoezi zima la utoaji elimu maredioni na katika majukwaa mbalimbali.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Lindi mhe.Maria Amos Batulaine wa kwanza kulia akiambataana na waheshimiwa wengine wawili akiwa redio mashujaa kutoa wito kwa wananchi mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi katika mabanda ya  utoaji elimu.

Msaidizi wa kumbukumbu Bi. Mwanakombo Ally akitoa elimu juu ya hatua zinazotakiwa kufuatwa wakati wa ufunguaji wa shauri kwa mmoja wa wateja aliyewasilisha hoja ya kutaka kujua  hatua za ufunguaji wa shauri.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mwanzo Nga’pa Mhe. Patricia Mombo akiwasilisha mada kwa wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi Lindi Mjini.

Zoezi la kupanda miti ni moja kati ya mambo yanayofanywa katika wiki hii ya sheria Mkoa wa Lindi.

Zoezi la kupanda miti ni moja kati ya mambo yanayofanywa katika wiki hii ya sheria Mkoa wa Lindi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mwanzo Lindi Mjini Mhe.Illuminata Lutakana akitoa elimu kwa moja kati ya wateja waliofika kupata huduma ya elimu katika banda la Mahakama.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni