Jumatatu, 26 Februari 2024

JAJI MANSOOR AWAITA WATUMISHI MEZANI KUJADILIANA

Na Evelina Odemba – Mahakama, Morogoro

 

Ikiwa ni wiki takribani tatu zimepita tangu kuadhimishwa kilele cha wiki ya sheria Kanda ya Morogoro na kote Nchini, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Latifa Mansoor amekutana na watumishi ili kufanya tathimini na kupeana mikakati.

 

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mansoor aliwapongeza watumishi hao wa Mahakama kwa kujitoa kwao kuwajibika katika majukumu waliyokabidhiwa ili kuhakikisha maadhimisho yanafana.

 

“Niwapongeze Majaji Kanda ya Morogoro, watendaji na watumishi wenzangu, hakika mmefanya kazi kubwa na nzuri, naamini baada ya hapa tutaenda kujipanga vyema ili wiki ya sheria ijayo kusiwepo na changamoto zilizobainishwa hapa,” alisema.

 

Aidha, Jaji Mansoor alisisitiza suala la uwajibikaji kwa kila mtumishi wa Mahakama na kueleza kuwa inawapasa kuwa na ushirikiano, umoja na 

uwajibikaji.

 

Aliongeza kuwa kila mtumishi yupo kwa jukumu moja kubwa la kumuhudumia mwananchi kwa usahihi na kwa wakati ili kuhakikisha wanaipeperusha vyema bendera ya Mahakama ya Tanzania kote nchini.

 

“Kila mmoja wetu hapa anatakiwa kuufahamu vyema mpango makakati wa Mahakama na kuuishi, tukifanya hivyo wote tutakwenda sambamba na dira ya 

Mahakama inavyotutaka.

 

“…mtumishi yeyote atakayekwenda kinyume na maadili hatofumbiwa macho kwa kuwa atakuwa anatukwamisha kufikia marengo yetu tuliyojiwekea sisi kama Mahakama kupitia mapango makakati wetu,” alihitisha Mhe. Mansoor.

 

Naye Naibu Msajili Mfawidhi, Mhe. Fadhili Mbelwa alipata wasaa wa kuwapitisha watumishi hao katika baadhi ya vipengele vya Mpango Mkakati wa Mahakama.

 

Aligusia kuwa maboresho makubwa yanayoonekana yamefanywa ni sehemu ya mkakati huo, hivyo kila mtumishi ana wajibu wa kuunga mkono kwa kuhakikisha anatekeleza majukumu yake kwa haki na usawa na kwa wakati.

 


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Latifa 

Mansoor akizungumza wakati wa kikao na watumishi wa Mahakama (hawapo pichani).

 

Kutoka katika kikao cha watumishi wa Mahakama Kanda ya Morogoro kulia ni

Jaji Mfawidhi, Mhe. Latifa Mansoor, kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Hadija Kinyaka na aliyekaa kwa mbele ni Naibu Msajili, Mhe. Fadhili Mbelwa.

 
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Fadhili Mbelwa akizungumzia mpango mkakati wa Mahakama ya Tanzania wakati wa kikao cha watumishi wa Mahakama Kanda ya Morogoro.

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Susan Kihawa akifuatilia kikao.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Bw. Ahemd Ng’eni akizungumza masuala ya kiutawala wakati wa kikao hicho.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Mhe. Asha Waziri (kulia) na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya, Mhe. Mary Kallomo (kushoto) wakifuatilia kikao.

Afisa Tawala wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro, Bw. Emmanuel Machimo akitoa mchango wake wakati wa kikao.

Watumishi wa Mahakama Kanda ya Morogoro wakifuatilia kikao.


Kikao kikiendelea.


Meza kuu ikifuatilia kikao.

(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)

 























 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni