Jumatatu, 19 Februari 2024

KUWENI NA DESTURI YA KUPANDA MITI MAENEO YANAYOWAZUNGUKA: JAJI MKUU

Na. Stephen Kapiga-Mahakama, Mwanza.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma tarehe 15 Februari 2024 aliwaongoza Majaji wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania wanaondelea na vikao vya Mashauri ya Mahakama ya Rufani katika zoezi la upandaji miti ya matunda katika eneo la viwanja vya jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Jijini Mwanza.


Mhe. Prof. Juma katika zoezi hilo aliongozwa na mwenyeji wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mwanza Mhe.Dkt Ntemi Kilekamajenga pamoja na watumishi wa Mahakama wanaofanya kazi katika jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki jijini Mwanza na kupanda jumla ya miti sita ya matunda katika zoezi hilo. 

“Nimefurahi kuweza kushiriki katika zoezi hili kwani naamini miti ni moja ya kumbukumbu nzuri inayoishi, nawasihi sana muweze kupanda miti kwa wingi katika maeneo yenu kwani ni moja ya njia ya utunzaji wa mazingira katika maeneo yetu ya kazi hata majumbani”, alisema Mhe.Prof. Juma.


Katika upandaji miti huyo uliwashirikisha Majaji wa Mahakama ya Rufani walioko katika vikao vya usikilizaji wa mashauri ya Mahakama ya Rufani Kanda ya Mwanza ambao ni Jaji wa Rufani ya Tanzania, Mhe. Rehema Mkuye, Mhe. Dkt. Mary Levira, Mhe. Lameck Mlacha, Mhe. Paul Ngwembe na Mhe. Abrahamu Mwampashi.


Waheshimiwa Majaji hao, wanaendelea na vikao vya kusikiliza mashauri ya Mahakama ya Rufani katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania masijala ndogo ya mwanza ambapo jumla ya Mashauri 78 yanatarajiwa kusikilizwa na kutolewa uamuzi na kati ya Mashauri hayo Mashauri ya jinai ni 16, Mashauri ya madai ni 16, Mashauri ya maombi ya madai ni 44 na Mashauri ya maombi ya jinai ni 2.


Vikao hivyo vinatarajiwa kufikia tamati siku ya tarehe 23 Februari, 2024 na hivyo kuendelea na kasi ya uamuzi wa mashauri katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania kwa lengo la kuendana na mpango mkakati wa Mahakama ya Tanzania wa mwaka 2020/2021-2024/2025 hasa katika nguzo yake ya pili ya kuhakikisha kuwa upatikanaji wa haki kwa wakati na kwa wote.

Jaji Mkuu Tanzania Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza zoezi lilifanyika tarehe 15 februari 2024.

Jaji Mkuu Tanzania Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Rehema Mkuye akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini Mwanza

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Rehema Mkuye akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini Mwanza.


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Dkt. Mary Levira akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Dkt. Mary Levira akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Abraham Mwampashi akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Abraham Mwampashi akipanda mti wa matunda ya machungwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lameck Mlacha akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lameck Mlacha akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lameck Mlacha akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Lameck Mlacha akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Paul Ngwembe akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Paul Ngwembe akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza.

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Paul Ngwembe akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza


Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Paul Ngwembe akipanda mti wa matunda ya mparachichi kama kumbukumbu katika eneo la kituo jumuishi cha utoaji haki Jijini mwanza


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni