Jumanne, 20 Februari 2024

MAHAKAMA KUTOA MAFUNZO YA MATUMIZI MSINGI YA TEHAMA KWA WATUMISHI WAPATAO 1,829

Na. Ahmedi Yusufu na Innocent kansha.

Mahakama ya Tanzania imeanza kutoa mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) kwa Watumishi wake 1,829 ambapo 1,324 ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na 505 ni Waandishi Waendesha ofisi.

Mafunzo hayo ya wiki saba yameanza kutolewa  tarehe 19 Februari, 2024 katika mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma na yamefunguliwa  na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Bw. Victor Kategere kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania  Prof. Elisante Ole Gabriel.

Pia mafunzo haya yamefunguliwa kwa pamoja ambapo Dar es Salaam yanafanyika katika ukumbi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa na Dodoma ni katika Ukumbi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania.

Akihutubia katika mafunzo haya, Bw. Kategere ambaye alizungumza kwa njia ya mtandao na washiriki waliopo Dar es Salaam huku yeye akiwa jijini Dodoma, amewataka washiriki wahakikishe wanatoka kwenye mafunzo hayo wakiwa na dhamira ya dhati ya kwenda kutumia mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufanya kazi.

Pia, amewaambia washiriki hao: "Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na Waandishi waendesha ofisi ni wadau muhimu katika matumizi ya mifumo kama e-case Management na e-office. Hivyo haitarajiwi msaidizi wa kumbukumbu kwa vyovyote kutoa kisingizio cha kutokujua kutumia mifumo hiyo."

Mafunzo haya yanatolewa na Mahakama ya Tanzania kupitia Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto na yanaendeshwa na wataalamu kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu alianza kwa kutoa, historia fupi ya kwanini mafunzo hayo yanafanyika.

“Mwaka 2021/22, Mahakama ilifanya zoezi la kutathmini Utayari wa Watumishi wa Mahakama katika kutumia TEHAMA na Vifaa vya TEHAMA. Zoezi lilibaini uwepo wa miundombinu pamoja na uwepo wa watumishi wanaopenda kutumia TEHAMA katika kazi zao. Hata hivyo, changamoto kubwa ilikuwa ni ukosefu wa maarifa na ujuzi miongoni mwa watumishi wa Mahakama likiwemo kundi hili”, amesema Bi. Ngungulu

Aidha, Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa, wakati wa Baraza la Wafanyakazi la mwaka 2023 lililofanyika Mei, 2023 jijini Dodoma, suala la kujenga uwezo katika matumizi ya digitali yalijadiliwa na kuelekezwa kuwa suala hili lifanyike kwa watumishi wote hasa wakati huu ambao Mahakama inaelekea kwenye Mahakama Mtandao. Hivyo, maandalizi kwa ajili ya mafunzo haya yakaanza mara moja na leo tumeanza kazi ya kuwawezesha watumishi katika eneo hilo.

Bi. Ngungulu ameongeza kuwa, mafunzo hayo yenye idadi kubwa ya washiriki, ni mradi mkubwa kuwahi kufanyika na ambao utagharimu takribani 2.5 Bilioni, ambapo matokeo ya mafunzo haya, yataweka njia kwa makundi mengine ya watumishi kuwezeshwa kwenye mafunzo kama hayo.

“Nitoe rai kwa washiriki kuzingatia mafunzo haya na kuhakikisha kuwa maarifa na ujuzi utakaopatikana kutokana na mafunzo, unatumika vizuri katika kuharakisha utoaji huduma na wenye tija kwa ujumla kwenye maeneo yao”, amesisitiza Mkurugenzi Msaidiszi huyo.  

Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama (IJA) Mhe. Dkt. Patricia Kisinda akizungumza akiwa Dar es Salaam, amewaomba washiriki kutumia vizuri mafunzo hayo ili kuboresha maarifa yao katika matumizi ya TEHAMA.

Naye, Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) jijini Dar es salaam, Dkt. Ernest Mabonesho amesema kuwa kwa sasa Utumishi wa umma unahitaji mtu mwenye ujuzi wa matumizi ya TEHAMA ili kuweza kutenda kazi zake kwa urahisi na kuzaa matokeo bora. 

Miongoni mwa malengo ya mafunzo haya ni kuwapatia na kukuza maarifa na ujuzi wa washiriki ili kuweza kutumia mifumo ya kidigiti katika kazi zao za Kimahakama, ikizingatiwa kuwa kwa sasa utendaji kazi wa Mahakama unaelekea zaidi mtandaoni (e-judiciary).

Haya ni mafunzo ya awali baada ya mtaala kuandaliwa na IJA na kupitishwa na Mahakama ya Tanzania na yanafadhiliwa na Serikali ya Tanzania kupitia mkopo wa Benki ya Dunia ikiwa ni utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania.

Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Bw. Victor Kategere akihutubia wakati wa ufunguzi wa mafumzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) kwa Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi.   Amefungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania  Prof. Elisante Ole Gabriel, katika ukumbi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma tarehe 19 Feberuari, 2024. 

Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu akitoa neno la ukaribisho kabla ya uzinduzi wa mafunzo hayo jijini Dar es salaam.

Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama (IJA) Mhe. Dkt. Patricia Kisinda akizungumza wakati wa kutoa salamu fupi za Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kabla ya uzinduzi wa mafunzo hayo.

Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) jijini Dar es salaam, Dkt. Ernest Mabonesho akitoa neno la utangulizi kwa niaba ya Chuo hicho.
 Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Bw. Victor Kategere (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) kwa Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha Ofisi ambayo yanafanyika Dar es Salaam na Dodoma.  Wengine ni (kwanza kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi Utawala Mahakama ya Tanzania Bw. Stephen Magoha na wa (kwanza kulia) ni Mratibu wa mafunzo kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA), Bw. Nuhu Mtekele.





Mashauri mwelekezi kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC),  Bw. Charles Magaya akiwezesha mada katika Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambayo yanatolewa kwa Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi jijini Dodoma.   


Washiriki wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambao ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi wakifuatilia mada kutoka kwa mwezeshaji. 


Washiriki wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambao ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi wakifuatilia mada kutoka kwa mwezeshaji. 

Washiriki wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambao ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi wakifuatilia mada kutoka kwa mwezeshaji.
 
Washiriki wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambao ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama, chuo cha uongozi wa mahakama Lushoto na Mkuu wa chuo cha utumishi wa umma jijini Dar es salaam (magogoni).Katikati walioketi ni Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) jijini Dar es salaam, Dkt. Ernest Mabonesho,kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu na kulia ni Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama (IJA) Mhe. Dkt. Patricia Kisinda. 
 
Washiriki wa Mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) ambao ni Wasaidizi wa kumbukumbu wa Mahakama na  Waandishi Waendesha ofisi wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama, chuo cha uongozi wa mahakama Lushoto na Mkuu wa chuo cha utumishi wa umma jijini Dar es salaam (magogoni). Katikati walioketi ni Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) jijini Dar es salaam, Dkt. Ernest Mabonesho,kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu na kulia ni Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama (IJA) Mhe. Dkt. Patricia Kisinda.
 

Wakufunzi na Sekretariati ya mafunzo ya matumizi ya msingi ya stadi za kidigiti (Basic Digital skills) wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mahakama, chuo cha uongozi wa mahakama Lushoto na Mkuu wa chuo cha utumishi wa umma jijini Dar es salaam (magogoni). Katikati walioketi ni Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) jijini Dar es salaam, Dkt. Ernest Mabonesho,kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu na kulia ni Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama (IJA) Mhe. Dkt. Patricia Kisinda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni