Na Innocent Kansha – Mahakama.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ametoa rai kwa ujumbe wa Tume ya
Usuluhishi na Uamuzi kutumia jukwaa la mkutano wa mwaka na kuwajumuisha Majaji
Wafadhidhi, Naibu Wasajili na wawakilishi wa Tume waliopo nchini ili kujadili
changamoto na kuzitafutia ufumbuzi kupitia jukwaa hilo ili kusaidia namna bora
ya kuboresha utendaji kazi.
Ameyasema
hayo leo tarehe 03 Mei, 2024 alipotembelewa Ofisini kwake jijini Dar es salaam
na Ujumbe wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwa ajili ya kujitambulisha na
kuwasilisha salamu za Kamishana wa Tume hiyo.
“Nikiri
tumekuwa tukikutana mara kwa mara lakini katika mwavuli wa shughuli nyingine
tofauti ambazo hazitukutanishi kujadili mambo yanayohusu Mahakama na Tume
hususani masuala ya utendaji kazi wetu na changamoto tunazozipitia na kuzipatia
utatuzi wa kuimarisha utendaji kazi”, amesema Jaji Mkuu.
Mhe.
Prof. Juma amesema ni vema Tume inakaona uwezekano wa kutumia kalenda ya kabla
ya Siku ya kilele cha sheria nchini kwa maana ya wiki ya sheria kila mwaka.
Tume ikaandaa mkutano wa jukwaa la wadau na kutumia fursa hiyo kujadili mambo
mbalimbali ya kuboresha shughuli za Tume kutoka kwa wadau ili kuboresha
utendaji kazi.
Mhe.
Prof. Juma ameongeza kuwa, jukwaa hilo la kila mwaka linapaswa kuwa na kauli mbiu
na kualika wadau kutoa mada na mawasilisho na mawasilisho mazuri yatoke hasa kwa
wale wadau wanaofanya kazi na kushughulika na matatizo zaidi siyo kutumia wanataaluma
wanaofanya kazi kwa nadhalia zaidi
“Nimependa
sana uono wako kwamba unapozungumzia uwekezaji shughuli zenu ni muhimu sana katika
kuboresha mazingira ya uwekezaji na pia zinalenga kuwajengea imani wakezaji
hasa pale migogoro inapotatuliwa kwa wakati na haki kutendeka”, ameongeza Jaji
Mkuu.
Jaji
Mkuu amesema uwekezaji unatengemea sehemu ambayo haina migogoro au ina utaratibu
wa usuluhishi wa migogoro unaoeleweka. Mwekezaji hataki aende sehemu ambayo
anajua kuna mifumo ya kutatua migogoro lakini haieleweki au kuna ucheleweshaji
hayo ni maeneo ya kuyazingatia katika vipaumbele vya Tume.
Kwa
upande wa eneo la teknolojia, Jaji Mkuu akachua nafsi hiyo kuipongeza Tume kwa jitihada
za kusimika mifumo ya kitehama itakayowasaidia kuendesha shughuli za utatuzi wa
migogoro hasa matumizi ya mkutano mtandao utakaorahisisha uzikilizaji na utatuzi
wa migogoro ya kazi hata pale wasipokuwa na wawakilishi wao kwa kutumia ofisi
za taasisi nyingine zenye miundombinu wezeshi.
Jaji
Mkuu amesema lengo vilevile la Tume ni kupunguza mashauri ya mapitio
yanayowasilishwa mahakamani kwani migogoro ikiweza kuishia kwenye ngazi ya Tume
mazingira ya utatuzi wa migogoro itakuwa imeimarika zaidi, kwani mahakamani
mdau anachua muda mrefu zaidi kwa wastani wa miaka mitatu hadi nne shauri
kumalizika. Wakati mwingine shauri linafika hadi Mahakama ya Rufani na kuamriwa
likaanze upya hali hiyo siyo nzuri kabisa hivyo Tume ikiimarisha utatuzi wa
migogoro wananchi watapata nafuu kubwa.
“Nahaidi
nitaendelea kuwasemea zaidi kwenye majukwaa mbalimbali kwani natambua umuhimu
wa Tume ya usuluhishi na uamuzi na pia napenda sana Wizara itambue umuhimu wenu,”
amesisitiza Jaji Mkuu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya
Usuluhishi na Uamuzi Wakili Usekelege Mpulla kwa niaba ya
Kamishna wa Tume hiyo pamoja na salamu amemweleza Jaji Mkuu Mhe. Prof. Juma
kuwa hivi karibuni Tume ilisaini makubaliano ya awali na Mahakama ya kubadilishana
nyaraka na kushirikiana katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji na kwa kupitia
hiyo Tume itakuwa ikishirikishana na Mahakama kutoa taarifa muhimu na kwa
uharaka ikiwemo wito wa majalada ya mashauri na mengineyo yanayofanya kuongeza
ufanisi katika utendaji na Mhimili.
“Mhe. Jaji Mkuu tumeona pia tukushirikishe
mikakati ya Tume uisikie na vivile tutakuandikia ili ije kwa ajili ya maelekezo
mbalimbali. Tunayo mikakati mbalimbali ya kuweza kuboresha utatuzi wa migogoro
ya kikazi moja wapo ikiwa ni kuongeza kasi na ufanisi katika utatuzi wa
migogoro na msisitizo wetu ikiwa ni usuluhishi ambao pia ni msisitizo wako”,
ameongeza Mkurungezi Mpulla.
Mkurugenzi
Mpulla amesema hivi sasa Tume inaendelea na zoezi la usimikaji wa mifumo ya
kielektroniki ya utatuzi wa migogoro na usajili kwa njia ya kielektroniki na
zoezi lipo katika hatua ya mwisho ya kuzinduliwa ili kuanza kufanya kazi ikiwa
pamoja na kuendana na kasi ya mifumo ya uendeshaji wa mashauri ya kimahakama.
Mkakati
mwingine ni kuimarisha ushirikiano na wadau ikiwa ni pamoja na Mahakama ambao
ni wadau muhimu katika shughuli za utatuzi na uamuzi wa migogoro ya kazi.
Pia,
Tume imesaini makubaliano ya awali na Kituo cha Uwekezaji nchini kwani Kituo
hicho kazi yake kubwa ni uwashawi wawekezaji kuwekeza mitaji nchini, na
wawekezaji ndiyo waajiri na ndiyo wazalishaji wa migogoro ya kikazi. Kufanya
kazi na Kituo kwa pamoja kunalenga kushirikiana na kutatua kero mbalimbali za
migogoro ya kazi kwa hao wawekezaji.
Aidha,
Mkurungezi Mpulla amesema mkakati mwingine ni kuomba Serikali kuwezeshwa kupata
magari yatayotumika kama Mahakama Inayotembea kwa ajili ya kuwafikia wananchi
wengi wenye migogoro ya kazi hasa maeneo ya kimkakati ili kutoa huduma kwa
urahisi zaidi kwa wananchi.
Vilevile
maombi ya kuongezewa idadi ya wasuluhishi na waamuzi, kwa upande huo bado
rasilimali watu haitoshelezi mahitaji japo Serikali imekuwa ikiongeza lakini
siyo kwa kiwango cha kutosheleza mahijati ukilinganisha na migogoro
inayosajiliwa ili kuamuriwa kwa wakati, ameongeza Mkurungezi Mpulla.
“Utoaji
wa elimu kwa wadau wa Tume, tunatarajia kutoa elimu kwa wadu wetu kwani wakati
mwingine migogoro mingine inatokana ukosefu wa elimu ya kutosha ya utatuzi wa
migogoro ya kazi. Tume inatarajia kutumia vipindi vya televisheni kama
inavyofanya Mahakama ili kuwafikia wadau wengi zaidi,” amesisitiza Mkurugenzi
hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni