Na Paul Pascal-Mahakama, Moshi
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Moshi Mhe. Dkt. Lillian Mongella
ameungana na baadhi ya watumishi wa Mahakama kumjulia hali na kumfariji
mtumishi mwenzao aliyepatwa na janga la mafuriko mnamo usiku wa kuamkia tarehe
25 Aprili, 2024 nyumbani kwake mtaa wa Langoni kata ya Mji Mpya Wilaya ya
Moshi.
Mtumishi
huyo Bw. Mussa Mssekeni ambaye ni Mlinzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi
anayeishi katika mtaa wa Langoni Kata ya Mji Mpya Wilaya ya Moshi alikumbwa na
mafuriko hayo kutokana na mvua kubwa iliyopelekea kujaa kwa mto Rau na kuacha
familia nyingi katika Kata hiyo bila makazi na mahitaji ya kibinadamu.
Akizungumza
wakati wa kumfariji mtumishi huyo Mhe. Dkt. Mongella alisema, anamshukuru Mungu kwa
zawadi ya uhai aliowajalia hadi kufikia siku ya hiyo maana janga hilo
limeagharimu maisha ya watu, akamuomba mtumishi huyo kuwa na subra katika
kipindi hicho anachokwenda kuanza kuijenga familia upya hasa akizingatia anaanza
kujitafutia upya mahitaji kwa ajili ya maisha ya kila siku ya familia.
“Msifadhaike
kwa kupoteza vitu katika makazi yenu sisi ni sehemu ya familia hii. Ndiyo maana
leo tumefika hapa na mkono wa pole ili maisha yaweze kuendelea. Yatupasa pia
kuchukua taadhari pale tunapoona hali sio shwari kwa muktadha wa maisha yetu,
kama Kanda tunawapa pole sana kwa kadhia ya mafuriko”, alisema Mhe. Dkt. Mongella
Naye
Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi Bw. Paul Mushi alieleza kuwa vitu
mbalimbali vilivyowasilishwa kwa mtumishi huyo ni ishara ya umoja na upendo
uliopo baina ya Watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi.
“Ni
utaratibu tuliojijengea kusaidiana pale anapotokea mmoja wa watumishi anapatwa
na tatizo hivyo kwa siku ya leo kupitia michango ya watumishi wa Kanda hii
tumeweza kuwasilisha kwa mwenzetu vitu vya nyumbani kama Godoro, jiko, vyombo
vya kulia chakula, nguo za watoto, blaketi, sabuni pamoja na vyakula kama
mchele, unga, mafuta na sukari niwashukuru watumishi wenzangu kwa ushirikiano
huu mliouonyesha,” alisema Kaimu Mtendaji huyo.
Kaimu
Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Moshi Bw Paul Mushi (katikati mwenye t-shirt
nyeupe) akitoa salamu za pole wakati wa tukio la kumfariji mtumishi mussa
msekeni aliyekumbwa na mafuriko nyumbani kwake kata ya mji mpya moshi
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Moshi Mhe. Dkt. Lillian Mongella akimkabidhi vifaa mbalimbali vya matumizi ya nyumbani na chakula kwa mtumishi mussa msekeni aliyekumbwa na mafuriiko.
Sehemu
ya watumishi wakiwa wamebeba vifaa vya matumizi ya nyumbani kuelekea kumfariji
mtumishi mwenzao aliekumbwa na mafuriko nyumbani kwake mji mpya moshi
Sehemu
ya watumishi wakiwa wamebeba vifaa vya matumizi ya nyumbani kuelekea kumfariji
mtumishi mwenzao aliekumbwa na mafuriko nyumbani kwake mji mpya moshi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni