Na Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga
Baraza
la Wafanyakazi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga linalojuisha mikoa ya Sumbawanga
na Katavi lilikutana jana tarehe 02 Aprili, 2025 na kujadili mambo mbalimbali yanayohusu
watumishi hasa ushirikishwaji katika utoaji wa maamuzi, baraza hilo lilifanyika
katika Ukumbi wa Mahakama uliopo katika Jengo la Mahakama Kuu, Kanda ya
Sumbawanga.
Akizungumza
wakati wa kufungua Baraza hilo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Sumbawanga Mhe. Frederick Kapela Manyanda ambaye pia alikuwa Mwenyekiti
wa kikao hicho alisema, utaratibu wa kuwa na mabaraza unalenga kukuza uwazi na
ushirikishwaji katika maamuzi mbalimbali.
Aidha,
Mhe. Manyanda alihimiza menejimenti ya Mahakama Kanda ya Sumbawanga na Chama cha
wafanyakazi (TUGHE) kushirikiana kwa
pamoja katika kutatua kero mbalimbali za
watumishi ili kuongeza morali ya
watumishi ambao ni wachache na wanafanya kazi nyingi.
Vilevile,
wakati wa kikao hicho cha Baraza kulikuwa na uwasilishwaji wa mapitio ya
bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ambayo kwa upande wa
mkoa wa Katavi iliwasilishwa na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi Bw.
Epaphras A.Tenganamba na kwa upande wa Mkoa wa Rukwa iliwasilishwa na Afisa bajeti wa Mahakama Kuu,
Kanda ya Sumbawanga BiT. Irene T. Mlangwa.
Naye,
Katibu TUGHE mkoa wa Rukwa Bw. Amin R. Msambwa aliomba kutekelezwa kwa vikao
viwili vya Baraza la wafanyakazi kama sheria inavyoelekeza ambapo kikao cha
kwanza kijadili mambo ya bajeti na kikao cha pili kijadili utekekelezaji wa
bajeti na pia utekelezaji wa hoja za kiutumishi zilizoibuliwa kwenye mabaraza
yaliyopita
Wakati
wa Baraza hilo wajumbe walijadili masuala mbalimbali ikiwemo mapitio ya Bajeti,
ukomo wa bajeti, utekelezaji wa bajeti, changamoto za utekelezaji wa bajeti, kupokea
na kujadili hoja za watumishi na pia majibu na ufafanuzi ulitolewa na viongozi
mbalimbali.
Wajumbe
waliohudhuria Baraza hilo kwa pamoja walikubaliana na kuweka mikakati ya pamoja
ya kutekeleza wa shughuli mbalimbali ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi
na pia kuboresha baadhi ya mambo wakati wa Baraza lijalo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Frederick Kapela
Manyanda akiongoza kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga.
Mjumbe wa Baraza Bw. Jacob A. Mwakajengele akichangia hoja wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi Mahakama Kanda ya Sumbawanga.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu E. Essaba akichangia hoja
wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi kilichofanyika Mahakama Kuu, Kanda ya
Sumbawanga
Katibu
wa TUGHE mkoa wa Rukwa Bw. Amin R. Msambwa akichangia hoja wakati wa kikao cha
baraza la wafanyakazi Mahakama kuu Kanda ya Sumbawanga
Mtendaji
wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi Bw. Epaphras A.Tenganamba akiwasilisha
mapitio ya bajeti ya mwaka 2025/2026 kwa mkoa wa Katavi.
Afisa Bajeti wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbwanga Bi Irene T. Mlangwa akiwasilisha mapitio ya bajeti ya mwaka 2025/2026 kwa mkoa wa Rukwa
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi Mahakama kuu Kanda ya Sumbwanga wakisikiliza
(Habari Hii Imehariri na Innocent Kansha-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni