Na Fredrick Mahava – Mahakama, Sumbawanga
Menejimenti
ya Mahakama ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga jana tarehe 02 Aprili, 2025 imekutana
na kufanya kikao cha robo ya tatu ya mwaka ambacho kimefanyika katika ukumbi wa
Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga.
Akifungua
kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Fredrick
Manyanda ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho alisema vikao hivyo ni
muhimu sana na vimekuwa vikifanya kila robo ya mwaka na kutoa fursa ya kujadili
mambo mbalimbali ya kiutendaji kama vile shughuli mama ya uendeshaji wa
mashauri.
Naye,
Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu E. Essaba
aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mahakama katika Kanda hiyo
kwa kipindi cha kuanzia Julai 2024 hadi Machi 2025. Katika taarifa hiyo ambayo ilikuwa
imegawanyika katika sehemu mbili iliainisha masuala ya kiutawala na masuala ya uendeshaji
mashauri.
Kwa
upande wa masuala ya utawala, Bw. Essaba alisema kuwa, utekelezaji wa mambo
mbalimbali ya kiutawala kama vile utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2024/2025,
masuala ya kushughulikia madeni, masuala ya watumishi, majengo na viwanja vya
Mahakama, miradi ya ujenzi inayoendelea, vitendea kazi, uwekaji wa taarifa
kwenye mfumo wa Mahakama wa ramani (JMap) na ukusanyaji wa maduhuri kwa mwaka
fedha 2024/2025.
Vilevile,
kwa upande wa masuala ya mashauri Bw. Essaba alitoa takwimu za mashauri
yaliyofunguliwa, mashauri yaliyoamuliwa, mashauri yanayosubili kusikilizwa na
mashauri ya mlundikano yaliyopo katika kila ngazi ya Mahakama yani kuanzia
Mahakama Kuu hadi Mahakama za mwanzo na mikakati ya namna ya kuyashughulikia.
Aidha,
Mtendaji huyo, alielezea mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha kuanzia Julai
2024 hadi Machi 2025 ambayo ni kuwezesha kufanyika kwa vikao vya Mahakama Kuu, kupunguza
mlundikano wa mashauri, kuanzisha kitabu cha utendaji kazi wa mwaka, kupata
hati za kiwanja cha Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga na nyumba ya Jaji (Judges
lodges), kuwawezesha watumishi mbalimbali kuhudhuria mafunzo ya muda mfupi na
mrefu.
Pamoja
na hayo, Mtendaji huyo alisema kuwa, kwenye mafanikio changamoto pia mbalimbali
zinazoikabiri Mahakama Kanda ya Sumbawanga ambapo kubwa ni ufinyu wa bajeti za
kuendeshea mashauri, ufinyu wa bajeti ya matengenezo ya magari, ufinyu wa
bajeti ya kutosheleza stahiki na maslahi ya watumishi na pia uhaba wa vitendea
kazi.
Naye,
Jaji Mfawidhi ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa kikao hicho aliruhusu wajumbe wa
kikao hicho kutoa maoni, ushauri, mapendekezo kuhusu ajenda mbalimbali
zilizojadiliwa wakati wa kikao hicho kwani baadhi ya changamoto zilizowasilishwa
zipo ndani ya uwezo zikitafakariwa zinaweza kupata suluhisho.
Wajumbe
waliohudhuria kikao hicho cha menejimenti ambao ni viongozi kutoka mikoa ya
Rukwa na Katavi walitoa maoni, ushauri kuhusu masuala mbalimbali
yaliyowasilishwa kwenye kikao na kuahidi kwenda kutekeleza yote yaliopitishwa
na kikao hicho.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda
akifungua kikao cha menimenti.
Wajumbe
wa kikao cha menejimenti Kanda ya Sumbawanga wakisikiliza taarifa inayotolewa
wakati wa kikao
Mtendaji
wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu E. Essaba akitoa taarifa ya
utekelezaji kwa kipindi cha kuanzia Julai 2024 hadi Machi 2025.
Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni