Na ARAPHA RUSHEKE- Mahakama, Dodoma
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Joseph
Mlyambina jana tarehe 23 Aprili, 2025 ameongoza Kikao kazi cha watumishi wa
Mahakama ya Tanzania kutoka sehemu mbalimbali wakiwemo waheshimiwa Majaji Wafawidhi,
Majaji, Naibu wasajili, Mahakimu, Wasaidizi wa sheria wa Majaji, watendaji wa
Mahakama na viongozi mbalimbali wataasisi za kiserikali zinazofanya kazi katika
mnyororo wa Mahakama kazi.
Kikao
hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wakala wa Usalama na Afya
Mahali pa Kazi (OSHA) uliopo tambukareli jijini Dodoma
Akizungumza
wakati wa neno la utangulizi wa Kikao hicho, Mhe. Dkt. Mlyambina alieleza kuwa Mafunzo
haya ni sehemu ya mwendelezo wa ushirikiano mwema kati ya Mahakama na OSHA
ushirikiano ulioanza kuimarika tangu kufanyika kwa mafunzo ya awali
yaliyohusisha Watumishi wenye ulemavu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali na
Kanda tofauti za Mahakama.
“Awamu
hii ya pili, tunajivunia kuwahusisha viongozi wa Mahakama, Ofisi ya Mkurugenzi
wa Mashtaka, Ofisi ya kamishina wa Kazi, CMA pamoja na viongozi kutoka OSHA,
jambo ambalo linadhihirisha dhamira ya dhati ya Muhimili wa Mahakama na
Serikali katika kuboresha mazingira ya kazi na huduma kwa wananchi. Ushirikiano
huu ni utekelezaji wa Nguzo ya Tatu ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya mwaka
2020/2021– 2024/2025, inayolenga kuimarisha imani ya wananchi kwa Mahakama
pamoja na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za Mahakama,” Jaji Mfawidhi huyo
alisema.
Aliendelea
kubainisha kuwa katika dunia ya sasa inayobadilika kwa kasi, maendeleo ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yameleta mapinduzi makubwa katika
sekta mbalimbali, ikiwemo Sekta ya Haki-Kazi. Matumizi ya Akili Unde
(Artificial Intelligence – AI) ni nyenzo muhimu ya kuongeza tija, kupunguza
gharama za uendeshaji, na kuharakisha utoaji wa maamuzi kwa wakati. Ni kwa
msingi huo, kauli mbiu ya mafunzo haya inasema: "Nafasi ya Akili Unde
(Artificial Intelligence –AI) Mahali pa Kazi (Mapinduzi na Fursa)." Kauli
mbiu hii si tu inasisitiza umuhimu wa teknolojia, bali pia inatufungua macho
kuhusu nafasi ya AI katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, kuhakikisha
usalama wa watumishi, na kupunguza hatari kazini.
Katika
salamu zake za ukaribisho Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, vijana, Ajira
na Wenye ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameushukuru uongozi wa Mahakama ya
Tanzania kwa kundeleza ushirikiano mzuri na muhimili huo katika kutambua umuhimu
wa usalama mahala pakazi kupelekea kukubali watumishi kushiriki mafunzo hayo
ambayo yatawasaidi na kuwajengea uelewa washiriki katika masuala ya usalama na
afya waweze kutekeleza maşukumu yao yake kila siku kwa kuzingatia kanuni bora na
kujilinda dhidi ya viatarishi vya magonjwa na ajali mahala pa kazi.
Naye,
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi Hadija Mwenda aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo
kutumia fursa hiyo kujifunza vitu vingi na kwaweredi mkubwa.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina akitoa neno la ukaribisho wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya usalama mahala pa kazi kwa watumishi wa mahakama na taasisi za mnyororo wa Mahakama Kazi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, vijana, Ajira na Wenye ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni