Jumanne, 8 Aprili 2025

JAJI MFAWIDHI TANGA AONGOZA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Na MUSSA MWINJUMA-Mahakama Kuu Tanga

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tanga, Mhe. Katarina Revocati Mteule hivi karibuni aliongoza Baraza la Wafanyakazi kwenye Kanda hiyo kujadili mambo mbalimnbali ya kiutendaji.

Akifungua mkutano wa Baraza hilo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Wazi wa Mahakama Kuu Tanga, Mhe. Mteule aliwashukuru wajumbe wote kufika kwa wakati pamoja na kwamba wengine wanatoka mbali.

Mhe. Jaji Katarina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo aliwakumbusha wajumbe umuhimu wa uwepo wa Baraza hilo kwani ni jukwaa la kujadili mambo mbalimbali muhimu yanayowahusu wafanyakazi.

 “Baraza la Wafanyakazi ni chombo ambacho wajumbe hutoa maoni, ushauri, mapendekezo na hata kukosoa kwa niaba ya Watumishi wengine ambao hawako hapa ili michango hiyo iingie kwenye utekelezaji wa shughuli za Mahakama, usiwe hapa kwa ajili ya kuongea matatizo yako binafsi ya kiutumishi,” alisema

Naye Afisa Kazi, Bw. Juma Mkali aliwapitisha wajumbe kwenye umuhimu,d humuni la mabaraza ya wafanyakazi. Pia aliwapitisha katika sheria mbalimbali za uundwaji wa mabaraza na kazi zake, ikiwemo ushauri juu ya maslahi ya wafanyakazi, utaratibu wa vyeo na nidhamu, kupokea na kujadili mapato na matumizi ya Taasisi.

Katika mkutano huo kulifanyika uchaguzi wa Katibu na Naibu Katibu kwa mujibu wa sheria za uundwaji wa baraza zinavyotaka ambapo Bw. Alinani Mwaiswelo alichaguliwa kuwa Katibu na Mhe. Bahati Manongi akiwa Naibu Katibu. Naye Bw. Farid Mnyamike ambaye ni Afisa Utumishi wa Kanda hiyo alichaguliwa kuwa mwakilishi wa Wafanyakazi katika Baraza la Wafanyakazi Taifa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tanga, Mhe. Katarina Revocati Mteule (katikati) akiongoza kikao cha Baraza la Wafanyakazi, kushoto kwake ni Jaji Messe Chaba na kulia kwake ni Katibu wa Baraza, Bw. Alinani Mwaiswelo na mwisho ni Naibu Katibu, Mhe. Bahati Manongi.

Sekretarieti ya Baraza la Wafanyakazi Mhe. Hudi Majid Hudi (mwenye suti) Naibu Msajili Mahakama Kuu Tanga na Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu Tanga, Bi Subira Mwishashi.

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Baraza wakimsikilzia Jaji Mfawidhi Katarina Revocati Mteule (hayupo pichani).

Wajumbe wa Baraza wakiendelea na kikao.

Bw. Farid Mnyamike ambaye amechaguliwa kuwa mwakilishi wa Wafanyakazi katika Baraza la Wafanyakazi Taifa akitoa shukrani zake kwa wajumbe baada ya kuchaguliwa.

Bi. Alice Haule ambaye ni Mwenyekiti TUGHE Taifa-Mahakama, akichangia mada katika mkutano huo.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni