Na INNOCENT KANSHA- Mahakama
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amempongeza Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake mkubwa wa
kufanikisha maboresho yaliyotekelezwa na yanayoendelea kutekelezwa na Mahakama
ya Tanzania kwa kuongeza idadi ya Majaji, Mahakimu na ujenzi wa miundombinu ya
kutolea huduma ya haki kwa wananchi.
Ameyasema
hayo, leo tarehe 05 Aprili, 2025 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa kihistoria
wa majengo matatu ya Mahakama likiwemo jengo la Makao Makuu ya Mahakama, jengo
la Tume ya Utumishi wa Mahakama na Majengo ya makazi ya Majaji.
Mhe.
Prof. Juma amenukuu hotuba ya Mhe. Dkt. Samia ya kwanza alipolihutubia Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza mara baada ya kuapishwa
kwake kuwa Rais, alisema "tutaenzi na kuendeleza mambo yote mazuri lakini pia
tutafanya mabadiliko pale inapobidi kwa lengo la kukuza ufanisi na tija katika kazi,".
Aidha,
Mhe. Prof. Juma ameongeza kuwa, Mahakama ya Tanzania ni wanufaika wakubwa sana
wa hiyo sehemu ya hotuba ya Mhe. Dkt. Samia kwa sababu Mahakama imeshuhudia
mapinduzi makubwa ya kuuwezesha Muhimili kutimiza ndoto ya miaka takribani 100
ya uwepo wa Mahakama nchini Tanzania.
Vilevile,
Mhe. Prof. Juma amesema kuwa, Mhe. Dkt. Samia aliahidi kwamba, "tutashirikiana
na Mhimili wa Mahakama katika kuimarisha mifumo ya utoaji haki ikiwemo
kuendeleza kujenga miundombinu ya Mahakama na tumeshudia katika kipindi cha
miaka minne Mahakama imejenga sana nchi nzima majengo ya kisasa ya kutolea
huduma za haki kwa wakati kwa wananchi,".
“Kuongeza
idadi ya Majaji na Mahakimu tumeona Rais akifanya hivyo, kukuza matumizi ya
TEHAMA ambayo Mhe. Dkt. Samia umejionea mwenyewe wakati wa ukaguzi wa jengo la
Makao Makuu ya Mahakama, namna ambavyo Mahakama inatumia TEHAMA, na pia wakati
ukiwa kwenye chumba maalum cha taarifa za kimahakama (Situation Room) na ulielezwa
na wataalum wetu kwamba, katika chumba hicho teknolojia hiyo Mahakama ilikwenda
kujifunza nchini Kazakhstan na ambao wao pia watakuja kujifunza kwetu kwa
sababu katika zama hizi za teknolojia kila mmoja anajaribu kumshinda mwenzake,”
amesisitiza Mhe. Prof. Juma.
Mhe. Prof. Juma amechukua wasaha huo kumshukuru sana Mhe. Dkt. Samia kwa hotuba yako "uliyoitoa Bungeni ilinisaidia sana, ilinipa nguvu na kuweza kwenda kuweka jiwe la msingi la jengo hili ambalo umelizindua leo. Hii simulizi imethibitisha kwamba Mhe. Dkt. Samia amejitoa kwa kiasi kikubwa kuhakikisha Mahakama inatimiza Dira yake ya Utoaji Haki sawa kwa wote na kwa wakati,".
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia mamia ya watanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa Majengo ya Mahakama iliyofanyika leo tarehe 05 Aprili, 2025 katika viwanja vya jengo la Makao Makuu ya Mahakama mtaa wa tambuka reli jijini Dodoma
(Picha na Innocent Kansha -Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni