Na
ASHA JUMA-Mahakama, Morogoro.
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewasili mkoani Morogoro
kuhudhuria mkutano mkuu wa Chama cha Majaji na Mahakimu (JMAT) utakaofanyika
siku ya Jumanne tarehe 15 April 2025 katika ukumbi wa Morena Hotel.
Jaji
Mkuu amewasili na treni ya umeme, maarufu SGR kutokea jijini Dodoma majira ya
saa 10:15 akipokelewa na mwenyeji wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Rose Ebrahimu na Majaji na Mahakimu wa Mahakama
Kanda ya Morogoro.,
Aidha,
Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro imempokea Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Mhe. Dkt Mustapher Mohamed Siyani, ambaye pia anatarajiwa kuhudhuria
mkutano huo.
Mkutano
wa Chama cha Mahakimu na Majaji unatarajia kufanya uchaguzi wa kupata viongozi wa
chama hicho kama vile Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makatibu katika ngazi za
juu za chama hicho.
Mkutano
huo ambapo awali ulitarajiwa kufanyika December 2024 ulisogezwa mbele kupisha
mkutano mkuu wa Majaji na Mahakimu wa Afrika Mashariki.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwasili mkoani Mororgoro
kwa treni ya umeme maarufu SGR kuhudhuria mkutano mkuu wa Chama cha Majaji na Mahakimu
Tanzania.
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akisaini kitabu cha wageni
katika stesheni ya Jakaya Kikwete alipowasili kuhudhuria mkutano huo.
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwa na Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Rose Ebrahim alipowasili
mkoani hapa.
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akiwa na Meneja Msaidizi wa Stesheni
ya Jakaya Kikwete, Bi. Getruda Masanja.
Jaji
kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt, Mustapher Mohamed Siyani akiwasili
mkoani Morogoro kuhudhuria mkutano wa Majaji na Mahakimu utakaofanyika Morena
Hotel Jumanne tarehe 15 April 2025.
Jaji
kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt, Mustapher Mohamed Siyani akisaini
kitabu cha wageni katika stesheni ya Jakaya Kikwete Mororgoro.
Jaji
kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt, Mustapher Mohamed Siyani akipokewa
na Majaji na Mahakimu wa Mahakama Kuu Kanda ya Mororgoro.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni