·
Wananchi
na wadau wafurahishwa na miundombinu ya kisasa ya Mahakama
Na Salum Tawani na Arapha Rusheke- Mahakama, Dodoma
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa, kwa mara ya kwanza
Mahakama ya Tanzania kuwa na Ofisi yake ya Makao Makuu ya Mahakama italeta tija
katika kutekeleza Majukumu yake kwa ufasaha.
Amezungumza
hayo katika uzinduzi wa Makao Makuu ya Mahakama uliofanyika katika eneo la
Tambuka Reli lililopo jijini Dodoma leo tarehe 05 Aprili, 2025.
“Kwa
uzinduzi wa majengo haya na mambo mengine ambayo yameonekana kwa Watanzania siyo
tu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
ametenda haki bali sisi Watanzania wote tumeona haki ambayo ameutendea Mhimili
wa Mahakama, Sekta ya Sheria na Sekta ya haki,” alisema Mhe. Dkt. Ndumbaro.
Aidha,
Waziri huyo amesema kuwa, amefurahishwa na ujenzi huo ambao umewashirikisha wazawa
na mchango wa maudhui ya asili (Local Content) wa wazawa kwenye kazi hiyo ni
asilimia kubwa, na asilimia 95 ya wataalam kwa maana wahandisi ni Watanzania na Mshauri elekezi ni
kampuni ya Kitanzania, hiyo ni hatua muhimu ya kuwajengea uwezo wataalam wa
ndani pamoja na makampuni ya wazawa, niwaombe Wizara na Taasisi zingine za
Kiserikali zizingatie umuhimu wa kuwashirikisha wazawa katika miradi mikubwa
kama ilivyofanya Mahakama.
Naye,
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule amesema imekuwa ni historia
kubwa kwa Dodoma ilikuwa na Mhimili miwili na leo Mhimili wa tatu
umekamilika na kuwa Makao Makuu ya Nchi, hiyo ni historia ya pekee ambayo
itakuandika Mhe. Rais katika vitabu vyote vya historia ya nchi ya Tanzania.
“Mhe
Rais dhamira yako ya kutaka haki tunaiona jinsi wakati wote umetamani Watanzania watendewe haki lakini jinsi ambavyo umetamani ardhi ya Tanzania
iandike haki kwa kila Mtanzania anayekanyaga katika nchi hii,” alisema Mhe.
Rosemary...
Mambo
haya Mhe. Rais tumeyaona ukiyasema kwa
maneno yako na tumeyasikia lakini
zaidi tumeona kwa vitendo ambavyo
umekuwa ukifanya vya kutenda haki, mfano
mdogo tu ulipoanzisha Mama Samia Msaada
wa Kisheria (Mama Samia Legal Aid) kupitia Wizara ya Katiba na Sheria ulitaka
hata watu wa chini wapate haki yao katika nchi yetu ya Tanzania,” alisema Mhe.
Rosemary
Mhe.
Senyamule amesema, jambo linaloonekana la kutoa fedha nyingi kwa ajili ya
utayari wa kujenga majengo kubwa ya kisasa ya Mahakama inaonyesha dhamira yako
ya dhati ya kutaka haki kwa kila Mtanzania.
Aidha,
Mkuu wa Mkoa huyo amempongeza Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma
kwa kutengeneza historia ya Mapinduzi makubwa katika Mhimili wa Mahakama ambao Dunia
inashuhudia majengo lakini amefanya na mambo mengine mengi ameyafanya katika
kipindi chake.
Ni
wazi kuwa, majengo yanayozinduliwa yatafanya watumiaji wafanye kazi kwa furaha,
amani na utulivu na kupelekea kuwatendea haki Watanzania wote ambao watapata
huduma katika eneo hilo.
Vilevile,
viongozi wa dini kwa nyakati tofauti wametoa pongezi kwa uongozi wa Mahakama
kwa hatua hiyo ya kuwa na majengo yao katika Mkoa wa Dodoma kwani imekuwa ni
faraja na jambo la kihistoria katika Nchi kushuhudia Majengo mazuri nay a kisasa
yakizinduliwa.
Wananchi
nao hawakuwa nyuma wameipongeza sana Mahakama ya Tanzania kwa kuboresha
miundombinu ya Mahakama na kushukuru kwa kupata majengo ya kihistoria katika
Mkoa wa Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb) akiongea neno la shukrani
wakati wa ufunguzi wa Majengo ya Mahakama leo tarehe 05 Aprili, 2025 jijini Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Sitaki
Senyamule akitoa sifa kemkem wakati akizungumza kwenye hafla ya ya ufunguzi wa majengo ya Mahakama .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni