Jumapili, 6 Aprili 2025

MAHAKIMU MBEYA WAHIMIZWA UMALIZAJI WA MASHAURI KWA WAKATI

Na Mwinga Mpoli – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga amewahimizwa Mahakimu kuhusu suala la usikilizaji na umalizaji wa mashauri kwa wakati na matumizi sahihi ya mifumo ya Mahakama lakini pia kuhakikisha wanaepuka kujaza mahabusu magereza ambao wana haki kudhaniniwa kwa mujibu wa sheria.

Mhe. Tiganga aliyasema hayo hivi karibuni katika kikao cha menejementi ya Kanda ya Mbeya kilichojumuisha Mkoa wa Mbeya na Mkoa Songwe na kusisistiza kufuata miongozo, kanuni, sera na sheria zilizopo ili kufanikisha utendaji kazi kwa ueledi na ufanisi wakati wa utoaji haki kwa wananchi.

“Tukumbuke kuwa tunalojukumu la kuhakikisha tunasikiliza mashauri na kuyamaliza kwa wakati. Aidha tuepuke kupeleka watuhumiwa mahabusu na magereza ambao wanaweza kupata dhamana au adhabu mbadala. Pia niwakumbushe tunapaswa kuhakikisha tuna matumizi sahihi ya mifumo yetu na kuwa tunaipitia mara kwa mara ili tuweze kutathmini utendaji kazi wetu,” alisema Jaji Tiganga.

Aidha, Mhe. Tiganga aliwasisitiza juu ya kusimamia utekelezaji wa mashauri na kama kutakuwa na changamoto wahakikishe wanatumia ubunifu ili kuhakikisha hawakwami katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Kikao kazi hicho kilihudhuriwa na wajumbe kutoka mkoa wa songwe na Mbeya ambao kwa pamoja wanaunda Kanda ya Mbeya.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga akieleza jambo katika kikao hicho.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (katikati) kulia ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Emily Temu na kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya Bi Mavis Miti katika kikao hicho.








  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni