Jumamosi, 12 Aprili 2025

WAJUMBE WA BARAZA WAPATIWA ELIMU MBALIMBALI

Na ARAPHA RUSHEKE –Mahakama, Dodoma

Katika kutimiza wajibu wake kisheria, Mahakama ya Tanzania iliandaa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi Taifa, ambalo linajumuisha wajumbe kutoka Mahakama mbalimbali za nchini Tanzania.

Baraza hilo ambalo lilifanyika katika Ukumbi wa PSSSF Jijini Dodoma kuanzia tarehe 11 na 12 April 2025 liliongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza hilo.

Wakiwa katika Baraza hilo, wajumbe walipatiwa elimu mbalimbali, ikiwemo kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa umma (PSSSF).

Mada nyingine ilikuwa ni maandalizi ya kustaafu katika utumishi na uongozi ambayo ilitolewa na Mhadhiri, mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe Dkt.Venance Shilingi, lakini pia wajumbe hao walipata mada ya afya ya akili kutoka kwa Bi Sadaka Ahmad Gandi.

Wajumbe walionyesha kufurahishwa na muitikio wa pamoja kuwa wamefarijika baada ya kuuliza maswali mbalimbali na kupatiwa majibu sahihi.

Mwenyekiti wa Baraza hilo aliwashukuru watoa mada wote pamoja na wajumbe kwa ushirikiano walioutoa tangu mwanzo mpaka kufikia kikomo.



 






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni