Jumatatu, 30 Juni 2025

JAJI MWAKAPEJE AFANYA ZIARA YA MAHAKAMA GEITA

Na DOTTO NKAJA-Mahakama, Geita

Hivi karibuni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Geita, Mhe. Griffin Mwakapeje alifanya ziara ya ukaguzi wa Mahakama kwenye Kanda hiyo ili kujionea maendeleo ya kiutenda, kuwaongezea maarifa katika utoaji haki Mahakimu na Watumishi wengine pamoja na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili.

Mhe. Mwakapeje alifanya ziara hiyo kwa niaba ya Jaji Mfawidhi, Mhe. Kevin Mhina kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita, Mahakama ya Wilaya Geita na Mahakama za Mwanzo Nyankumbu, Katoro, Bugando na Butundwe.

Akiwa katika ziara hiyo, Jaji Mwakapeje alijionea jinsi Mahakama hizo zinavyokwenda na kasi aliyoelekeza na Jaji Mfawidhi, ikiwemo kusikiliza mashauri kwa wakati na kwa kufuata misingi iliyowekwa.

Akizungumuza na Watumishi katika Mahakama hizo, Mhe. Mwakapeje aliwaasa kujiepukane na vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa upendo na ushirikiano.

Katika ziara hiyo, Jaji Mwakapeje aliambatana na Naibu Msajili, Mhe. Fredrick Lukuna, Mtendaji wa Mahakama Geita, Bi. Masalu Kisasila, Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita, Mhe. Clefas Waane, Kaimu Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Geita, Mhe. Bruno Bongole na Viongozi wengine.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Geita, Mhe. Griffin Mwakapeje akisaini kitabu cha wageni katika Mahakama ya Mwanzo Butundwe wilayani Geita.

Kaimu Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Geita, Mhe. Bruno Bongole akiwakaribisha timu ya ukaguzi iliyoongozwa na Jaji Mwakapeje katika Mahakama ya Mwanzo Katoro.

Jaji Mwakapeje akikagua majalada kwa njia ya mfumo katika Mahakama ya Mwanzo Katoro.

Watumishi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya Geita pamoja na Mahakama ya Mwanzo Nyankumbu wakiwa kwenye kikao na Jaji Mwakapeje.


 Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Geita, Mhe. Griffin Mwakapeje- katikati kwenye mstari wa kwanza pamoja na Viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Katoro wilayani Geita.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni